ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, October 13, 2018

MTUKUFU DKT. SYEDNA MUFADDAL SAIFUDDIN SAHEB AMALIZA ZIARA YAKE JIJINI MWANZA.



GSENGOtV

Octoba 12, 2018 Mkuu wa Jumuiya ya Dawoodi Bohra Duniani Mtukufu Dkt. Syedna Mufaddal Saifuddin Saheb (TUS) hatimaye amemaliza ziara yake ya siku 3 mkoani Mwanza.

Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella amemsindikiza Kiongozi huyo katika uwanja wa ndege jijini hapa.


Akiwa na msafara wake wenye watu takribani 25, kiongozi huyo amemaliza ziara yake kwa mafanikio, ambapo aliweka kambi yake ya mapumziko katika eneo la kitalii la Wag Hill Lodge liliyoko Luchelele wilayani Nyamagana.
Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella akimkabidhi  zawadi  Mkuu wa Jumuiya ya Dawoodi Bohra Duniani Mtukufu Dkt. Syedna Mufaddal Saifuddin Saheb picha ya kuchora ya ukutani yenye kuonesha mazingira ya jiwe la utalii lililoko kwenye mwambao wa Ziwa Victoria eneo la Kamanga, (Bismarck Rock) kama ishara ya kumbukumbu ya ziara yake mkoani hapa.

Ziara ya kiongozi huyo ililenga kutoa baraka kwa waumini wa Jumuiya ya Bohra, kushiriki nao ibada sanjari na kujionea hali ya mazingira ya kiutalii na vivutio vilivyopo mkoani Mwanza, adhma iliyotimizwa bila kukosa hata chembe. 

Mheshimiwa Mongella kamkabidhi Dkt. Syedna zawadi ya picha ya kuchora ya ukutani yenye kuonesha mazingira ya jiwe la utalii lililoko kwenye mwambao wa Ziwa Victoria eneo la Kamanga, nalizungumzia Bismarck Rock.

Mkoani Tabora ndiko uelekeo wa Kiongozi huyu Mkuu wa Jumuiya ya Dawoodi Bohra Duniani.
 
"Naaam Picha inazungumza.....Picha imemvutia.........."
Dakika chache kabla ya ndege iliyombeba Mkuu wa Jumuiya ya Dawoodi Bohra Duniani Mtukufu Dkt. Syedna Mufaddal Saifuddin Saheb na msafara wake kuondoka katika uwanja wa ndege wa Mwanza.


HATIMAYE WAMACHINGA WAMERIDHIA KWA AMANI KULIACHIA ENEO LA MMILIKI HALALI SAHARA



ZEPHANIA MANDIA/GSENGOtV

HATIMAYE wafanyabiashara waliokuwa wakifanya bishara zao katika eneo la kiwanja cha soko dogo la Sahara wamekubali kuliachia eneo hilo kuendelea na matumizi yaliyopanga na mwekezaji wake.

Mathias Charles Ndetto ndiye mmiliki halali wa kiwanja hicho namba 195 A BLOC U  Rwagasore  anasema amepata faraja kuona muafaka unapatikana na wafanyabiashara hao wanaondoka sasa kwa amani, tofauti na vile ilivyokuwa ikidhaniwa kwama 'pangechimbika'.

Halmashauri ya jiji pamoja na Serikali ya Mtaa baada ya kufanya ukaguzi na uhakiki kwa mabanda katika eneo la Serikali lililopo jirani na kiwanja hicho wamewapanga upya wamachinga kwenye maeneo yao huku wakilazimika kuzifunga baadhi ya njia ndogo za kupita wateja ili kuwapa nafasi wafanyabishara waliohamishwa nafasi ya kupanga biashara zao.  

“UMUHIMU WA MBOLEA NI PALE INAPOMFIKIA MKULIMA SHAMBANI SIO KUWA GHALANI’ DKT TIZEBA


Waziri wa Kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba akizungumza na wanachama wa chama cha Tuungane wakulima Interpises katika kijiji cha Mbugani kilichopo kata ya Itunundu Mkoani Iringa katika ziara ya kikazi ya kukagua hali ya upatikanaji wa mbolea katika mikoa ya Nyanda za juu kusini leo tarehe 12 Octoba 2018. (Picha Zote Na Mathias Canal-WK)
Waziri wa Kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba akikagua mfereji wa maji wa Mkombozi na Mboliboli Tarafa ya Pawaga Mkoani Iringa kwa ajili ya umwagiliaji wa mashamba ya mpunga katika ziara ya kikazi ya kukagua hali ya upatikanaji wa mbolea katika mikoa ya Nyanda za juu kusini leo tarehe 12 Octoba 2018.
Waziri wa Kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba akikagua mashamba ya mpunga alipotembelea Tarafa ya Pawaga Mkoani Iringa katika ziara ya kikazi ya kukagua hali ya upatikanaji wa mbolea katika mikoa ya Nyanda za juu kusini leo tarehe 12 Octoba 2018.
Waziri wa Kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba akikagua Ghala la kuhifadhi mpunga la Tuungane Wakulima Inteprises wakati akiwa katika ziara ya kikazi Mkoani Iringa kukagua hali ya upatikanaji wa mbolea katika mikoa ya Nyanda za juu kusini leo tarehe 12 Octoba 2018.
Waziri wa Kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba akikagua mashine ya kukoboa mpunga ya Chama cha Tuungane Wakulima Inteprises wakati akiwa katika ziara ya kikazi Mkoani Iringa kukagua hali ya upatikanaji wa mbolea katika mikoa ya Nyanda za juu kusini leo tarehe 12 Octoba 2018.

Na Mathias Canal-WK, Iringa

SERIKALI imesema itahakikisha mbolea inawafikia wakulima kwa wakati kabla ya kuanza msimu wa kilimo wa mwaka 2018/19 kwani umuhimu wa mbolea ni pale inapowafikia wakulima shambani sio kuhifadhiwa ghalani.

Katika msimu ujao Serikali imejipanga kuhakikisha kuwa wakulima wanapata mbolea na pembejeo nyingine katika maeneo yao wakati wote wanapohitaji ili kuondoa adha ya muda mrefu ya mbolea kuchelewa kuwafikia wakulima kwa wakati.

Waziri wa Kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba ametoa kauli hiyo leo tarehe 12 Octoba 2018 wakati akizungumza na wanachama wa chama cha Tuungane wakulima Interpises akiwa katika ziara ya kikazi kata ya Itunundu Mkoani Iringa kukagua hali ya upatikanaji wa mbolea katika mikoa ya Nyanda za juu kusini.

Dkt. Tizeba amesema kuwa ili kuboresha usambazaji wa pembejeo kwa wakulima katika msimu wa mwaka 2017/2018 mfumo wa ununuzi wa mbolea kwa pamoja (Bulk Procurement system- BPS) umeongeza upatikanaji wa mbolea kwa wingi, bei nafuu na wakati.

Aidha, kwa kutumia utaratibu huo bei za mbolea aina ya DAP na UREA zimepungua kwa wastani wa asilimia 30.

Akifafanua zaidi, Dkt Tizeba alisema kuwa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea (TFRA) inaendelea kufanya ukaguzi wa mara kwa mara na pindi ukiukwaji wa bei elekezi unapobainika hatua stahiki zinachukuliwa kwa wahusika.

” Endapo kama kuna mtu atapandisha gharama za mbolea kwa kupandisha bei maradufu zaidi ya bei elekezi serikali itamchukulia hatua haraka za kisheria atakayebainika ” Alikaririwa Dkt Tizeba

Katika kuimarisha sekta ya kilimo serikali imekuwa ikichukua hatua mbalimbali kuimarisha kilimo kwa kuwekeza katika pembejeo, mbolea na zana zinazoweza kuikuza sekta ya kilimo ili iweze kuchochea uchumi wa viwanda.

Kadhalika, Waziri Tizeba amewatoa hofu wakulima nchini kuwa kuna akiba ya mboleaya awali isiyopungua Tani 80,000 kwa ajili ya kupandia.

MWISHO

Friday, October 12, 2018

BAADA YA KUFANYA WIZI JIJINI DAR - POLISI MWANZA WANASA BASI LILILOKUWA LINATAKA KUCHINJWA



NA ZEPHANIA MANDIA/GSENGOtv

JESHI la polisi mkoa wa Mwanza limekamata watu wawili wanaosadikika kuwa ni majambazi wakitajwa kuiba gari lenye namba T 929 DCD aina ya HINO mali ya kampuni ya Sanu East Africa LTD ya Jijini Dar es salaam katika eneo la Kishiri - Igoma wilayani Nyamagana jijini Mwanza.

Akizungumza na vyombo mbalimbali vya habari mkoani hapa Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Mwanza, Jonathan Shanna amesema ukamataji huo umefanyika tarehe 11/10/2018 majira ya saa Kumi na Moja jioni. hii ni baada ya Jeshi lake kupata taarifa za kutoka kwa wasamaria wema, wazalendo wakipenyeza taarifa kwamba, kuna watu wameingia mkoani kwake na gari waliloliiba jijini Dar es salaam ambapo mara baada ya taarifa hiyo, Polisi walianza ufuatiliaji wa chocho kwa chocho na hatimaye kufanikiwa kukamata wezi hao wakiwa na gari hilo.

Kabla ya kukamatwa kwa gari hilo, taarifa zinaeleza kuwa ni mara mbili lilipelekwa kwenye gereji tofauti tofauti jijini hapa kwaajili ya kukatwakatwa vipande ili liuzwe kama spea na vyuma chakavu lakini ilishindikana mara baada ya wamiliki wa gereji hizo kukataa kufanya zoezi hilo kutokana na kuwa na maswali mengi yaliyokosa majibu yaliyozingirwa na hofu.


TANESCO YAALIKA WAWEKEZAJI WA VIWANDA, YASEMA UMEME UPO WA KUTOSHA NA KUSAZA

 Meneja wa Mradi Kinyerezi II, Mhandisi Stephens S.A.Manda (wakwanza kulia), akimtembeza Naibu Mkurugenzi wa TANESCO (usambazaji) Mhandisi Raymond Seya, (wapili kulia), kujionea maendeleo ya mradi w aumeme wa Kinyerezi II jijini Dar es Salaam leo Ijumaa Oktoba 12, 2018. 

NA K-VIS BLOG/Khalfan Said
SHIRIKA la Umeme Nchini TANESCO limesema liko tayari kupokea uwekezaji wa viwanda vya aina zote kwani hivi sasa kuna umeme wa kutosha, bora na wa uhakika. Hayo yamesemwa na Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO (Ugawaji), Mhandisi Raymond Seya, baada ya kukagua maendeleo ya mradi wa umeme  Kinyerezi II jijini Dar es Salaam, Ijumaa Oktoba 12, 2018. 

“Mradi unafikia mwisho sasa, kwasababu mashine zote zimeshafungwa na uwezo wa mashine hizi ni kuzalisha  Megawati 240, tunamalizia mambo madogo madogo kama ujenzi wa barabara na kupaka rangi lakini pia kujenga ofisi za wafanyakazi.” 

Alifafanua Mhandisi  Seya Tunataka kuwahakikishia wananchi uwekezaji huu mkubwa wenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 750 zote zikiwa zimetolewa na serikali umekamilika na tayari umeingizwa kwenye Gridi ya taifa. 

“Tunapenda kumshukuru sana Mhe. Rais wa serikali ya awamu ya tano Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuridhia kufadhili mradi tunawahakikishia sera ya awamu ya tano ya kujenga uchumi wa viwanda itatekeelezwa kikamilifu na sisi kama TANESCO tuko tayari kupokea uwekezaji wa viwanda vya aina zote.” Alisema. 

Alisema, tayari umeme huo umeingizwa kwenye gridi ya taifa na hadi sasa kwa ujumla kuna kiasi cha umeme kwenye gridi ya taifa Megawati 1500 na ukiangalia repoti za matumizi ya umeme kila siku tunakiuwa na ziada ya Megawati 250 hadi 160, Wikiendi inakuwa zaidi kwa sababu matumizi ya umeme yanapungua kwa hivyo yunapoongeza vyanzo hivi vya uzalishaji umeme tuanzidi mkuwa na uwezo wa kuunganisha wateja zaidi na kutoa huduma iliyo bora.” Alisema. Mhandisi Seya pia alitembelea mradi mwingine wa upanuzi wa Kinyerezi I ambapo miundombinu ya kusimika mashine iko tayari na kwamba zoezi la kufunga mashine hizo litaanza wakati wowote luanzia sasa. 

Akitoa taarifa ya utekelezaji wa miradi hiyo, Meneja wa Mradi Kinyerezi II, Mhandisi Stephens S.A.Manda Alisema miradi yote miwili ni miradi ya kimkakati na kwamba wakati mradi wa Kinyerezi II tayari umekamilika, mradi wa upanuzi wa Kinyerezi I, umefikia asilimia 70. “Mradi wa upanuzi wa Kinyerezi I, utakuwa na Megawati 185 ambapo Kinyerezi I yenyewe inazalisha umeme Megawati 150 na hivyo utafanya jumla ya Megawati 335 utakapokamilika Agosti mwakani.

“Kwa hiyo miradi yote hii itakapokamilika tunazungumzia jumla ya Megawati 575 zitakuwa zinazalishwa hapa Kinyerezi.” Alifafanua Mhandisi Mmanda. “Sasa hivi kwenye Gridi ya Taifa tunatosheleza mahitaji yote na tuna ziada, kwa hiyo tunachosema kama Shirika la umeme tunao umeme wa mkutosha na wawekezaji waje ili tuweze ili twende na falsafa ya Rais wetu ya kuwa na nchi yenye uchumi wa kati lakini zaidi sana nchi yenye uchumi wa viwanda.” Alsiema. Mhandisi Mmanda alibainisha kuwa Mradi wa upanuzi wa Kinyerezi I utakamilika Agosti mwakani.

 Meneja wa Mradi Kinyerezi II, Mhandisi Stephens S.A.Manda (wapili kulia), akimpatia maelezo Naibu Mkurugenzi Mtedaji wa TANESCO (usambazaji), Mhandisi Raymond Seya, kuhusu namna mitambo katika chumba cha udhibiti (Control room) inavyofanya kazi
 Meneja Miradi Mwandamizi  TANESCO, Mhandisi Emmanuel Manirabona, akikagua mitambo kwenye chumba cha udhibiti (Control room) cha Kinyerezi II leo Ijumaa Oktoba 12, 2018.
 Mhandisi Seya (kushoto), akiteta jambo na Mhandisi Mmanda.
 Naibu Mkurugenzi Mtedaji Shirika la Umeme nchini TANESCO anayeshughulikia usambazaji, Mhandisi Raymond Seya, (katikati), kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika hilo, akitembelea mradi wa umeme wa Kinyerezi II kujionea maendeleo ya utekelezaji wa mradi huo leo Ijumaa Oktoba 12, 2018. Kulia ni Meneja wa Mradi huo, Mhandisi Stephenes S.A Mmanda (kulia) na Kaimu Meneja Uhusiano wa Shirika hilo, Bi. Leila Muhaji,.
 Moja ya mitambo ambayo tayari imewasili ili kutekeleza mradi mwingine wa upanuzi wa Kinyerezi I.




Muonekano wa eneo itakapofungwa mitambo kwenye eneo la upanuzi wa mradi wa umeme Kinyerezi I hadi kufikia leo Ijumaa Oktoba 12, 2018.

WAFANYABIASHARA MWANZA WALIA NA RIBA ZA MABENKI.



NA ZEPHANIA MANDIA/GSENGOtV

KUELEKEA uchumi wa Kati wa Viwanda 2025 Wafanyabiashara watumiaji wa Taasisi za kibenki wameiomba Benki Kuu Nchini kupunguza kiwango cha riba kwa Taasisi hizo ili wafanyabiashara waweze kujikwamua kiuchumi kupitia mikopo inayotolewa na Taasisi hizo.

Hiki ni Kikao cha Wafanyabiashara kutoka Klabu ya NMB Mkoa wa Mwanza ambapo wamekutanishwa na Benki NMB, Lengo likiwa ni kuziainisha mafanikio na kutambua changamoto wanazokumbana nazo katika biashara zao na utoaji huduma ili kujikwamua kiuchumi.

AJIUWA KWA KUJIRUSHA TOKA GHOROFANI.


Mapema Leo asubuhi mtu mmoja aliyetambulika kama Afisa Usimamizi wa fedha nchini Kenya (PriceWaterhouseCoopers (PwC)) amefariki dunia baada ya kujirusha ghorofani toka kwenye  moja ya majengo mjini Nairobi.

Bwana huyo anakwenda kwa jina la Stephen Mumbo, Meneja msaidizi wa PwC. 

Mkuu wa polisi wilaya ya Kilimani mjini Nairobi Michael Muchiri amethibitisha kutokea kwa tukio hilo. “Alikuwa Meneja Msaidizi wa Upelelezi wa Uendeshaji na Ushauri wa Kitaifa katika kampuni,” Amesema Muchiri . 

Baada ya kupatiwa huduma ya kwanza, ripoti zinaonyesha kuwa Mumbo alikimbizwa Hospitali ya Aga Khan ili apatiwe matibabu ya huduma ya kwanza lakini alishindikana kutokana na majeraha yake kuwa makubwa


Bado haijulikani nini kinachoweza kumchochea kuchukua hatua hiyo ya kukatisha maisha yake yeye mwenyewe

#PWC #PriceWaterHouseCoopers #Suicide #Kenya #BreakingNews 

MANSOOR AFUNGUA BARABARA KWA MSHAHARA WAKE - ZAIDI KM 80



NA ZEPHANIA MANDIA/GSENGOtV

Wananchi wa jimbo la kwimba mkoani Mwanza, wamempongeza mhe.Shanif Mansoor, mbunge wa jimbo la kwimba, kwa juhudi zake za kuwaletea maendeleo wakazi wa kata ya shilembo kwa kuwafungulia barabara zaidi ya km.30 kwa kutumia posho ya mshahara wake.

Diwani wa kata ya shilembo mhe.Elias Garula, amesema zaidi ya miaka 5o tangu vijiji hivi viazishwe hawakuwahi kuona barabara wala gari katika maeneo hayo, wananchi wamesema kutokana na changamoto ya barabara, wanawake wengi wamepoteza maisha na watoto hasa wakati wakujifungua, kutokana na ukosefu wa miundombunu ya barabara ambapo magari yalishindwa kufika katika vijiji vya shilembo.

Wananchi wamempongeza MANSOOR, kwa jitihadazake binafsi za kuwafunguliya barabara hiyo,ambazo kwao ilikuwa ni ndoto kwani maendeleo yamechelewa kufika maeneo hayo kutokana na changamoto ya kukosekana kwa  barabara.

Ndalawa Magashi, ni mtendaji wa kata ya shilembo tarafa ya mwamashimba wilayani kwimba mkoani Mwanza, amema,shukuru kubwa kwa mhe.MASOOR,kwa kazi nzuri anayo ifanya kwa wananchi wa jimbo la kwimba, nakusema wabunge wengi wamepita kwenye jimbo la kwimba lakini MANSOOR,ni mbunge wa pekee, maarufu mbunge wa vitendo.

Aidha wanancha wa kata ya shilembo baada ya kuona Greda limefika katika kata hiyo,walionyesha furaha yao huku wakipiga kelele za vifijo na nderemo kwakuona greda limeanza kuchimba barabara hiyo, kwani wanafunzi pia kipindi cha masika wanapatashida kuvuka maeneo korofi na wengine kushindwa kuhudhuriya masomo.

Pia wananchi wa kata shilembo, wameomba serekali kuangalia barabara hiyo kwa jicho la tatu kuiwekea moramu na kalavati ili barabara hiyo iwe ya kudumu na endelevu, kwani itafungua maendeleo katika maeneo hayo vijiji vya shilembo.

Thursday, October 11, 2018

MBARONI KWA KUMBAKA NA KUMNYONGA MTOTO WA MIAKA NANE





Jeshi la polisi mkoani Mbeya linamshikilia mkazi wa kata ya Upendo wilayani Chunya Masanja Willy (25) kwa tuhuma za kumbaka mtoto mwenye umri wa miaka minane, Kwangu Bundala ambaye alikuwa mwanafunzi wa darasa la kwanza katika shule ya msingi Upendo kisha kumnyonga na kumuua.

Afisa Mtendaji wa kata ya Upendo, Lucas Alan Mwangala ambaye ndiye aliyetoa taarifa polisi kuhusiana na tukio hilo la ubakaji amesema wananchi baada ya kupata taarifa za kubakwa kwa mtoto huyo walishirikiana na polisi kumkamata mtuhumiwa na kumfikisha kituo cha polisi ili sheria iweze kuchukua mkondo wake.

KAULI YA KATIBU MKUU WA CCM YAMUIBUA SUMAYE.



Waziri Mkuu Mstaafu, Fredrick Sumaye ameunga mkono kauli ya Katibu Mkuu  wa CCM, Dkt. Bashiru Ally ya kuwa vitendo vya rushwa na kutowajibika vinasababisha watu kupuuzia uchaguzi na kuuona kama ni maigizo akidai kuwa kauli hiyo ni marudio.

Sumaye amesema kuwa ni kweli watu hawana imani na kura kwakuwa amezungumza Katibu Mkuu wa chama tawala hivyo amekubaliana na vyama vya upinzani maana jambo hilo wamekuwa wakilizungumzia mara kwa mara.

Sumaye amefunguka kuwa kwa kipindi cha kuanzia mwaka 2010 hadi sasa wananchi wamekuwa waoga kutokana na siasa za mihemko zilizoibuka hivi karibuni, tokea kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi mwaka 1992.

"Uchaguzi wa mwaka 2010 ambao Bashiru aliutumia kutolea mfano niliwahi kuzungumzia kipindi hicho mara tu baadaya kutangazwa kwa matokeo, kwakuwa CCM ilipata ushindi ambao ulikuwa finyu, kwakuwa asilimia ilikuwa 25 tu ya kura zilizoandikishwa", amesema Sumaye.

Sumaye ameongeza kuwa kauli ya Dkt. Bashiru isiishie hapo akishauri chama tawala pia kufuate yale aliyosema ili kurudisha imani kwa wapiga kura.

WAZIRI DR HUSSEIN MWINYI AZINDUA JENGO LA KISASA LA UTAWALA SHULE YA SEKONDARI KAWAWA MJINI MAFINGA

Waziri wa ulinzi na jeshi la kujenga taifa Dr Hussein Mwinyi akiwa na baadhi ya maafisa wa jeshi la JKT kikosi cha 841 KJ Mafinga pamoja na mkuu wa JKT Tanzania Maj Gen SM Busungu wakiwa kwenye picha ya pamoja kwenye jengo la utawala la shule ya sekondari Kawawa wakati wa uzinduzi wa jengo hilo.
Waziri wa ulinzi na jeshi la kujenga taifa Dr Hussein Mwinyi akiwa na baadhi ya maafisa wa jeshi la JKT kikosi cha 841 KJ Mafinga pamoja na mkuu wa jeshi ya JKT Tanzania Maj Gen SM Busungu wakiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi wa shule ya sekondari ya Kawawa iliyopo Mafinga Mkoani Iringa.
Waziri wa ulinzi na jeshi la kujenga taifa Dr Hussein Mwinyi akiwa na baadhi ya maafisa wa jeshi la JKT kikosi cha 841 KJ Mafinga pamoja na mkuu  JKT Tanzania Maj Gen SM Busungu wakiwa kwenye picha ya pamoja
Na hili ndio jengo la kisasa la utawala la shule ya sekondari ya kawawa lililofunguliwa na waziri wa ulinzi na jeshi la kujenga taifa Dr Hussein Mwinyi

NA FREDY MGUNDA,IRINGA. 
WAZIRI wa ulinzi na jeshi la kujenga taifa Dr Hussein Mwinyi ameupongeza uongozi wa shule ya sekondari ya Kawawa kwa ujenzi wa jengo la kisasa la utawala ambalo litachangia katika ufanisi bora wa kazi kwa walimu na wafanyakazi wote wa shule hiyo. 
Akizungumza wakati wa kuzindua jingo hilo la utawala waziri Mwinyi alisema kuwa jengo limejengwa kwa viwango ambavyo serikali ya awamu ya tano inataka na jingo hilo lina viwango vinavyotakiwa.
“Kwa kweli nisiwe mchoyo wa fadhila jengo hili limejengwa kwa kuzingatia ujenzi unaotakiwa na lina ramani ambayo itadumu kwa miaka mingi na itakuwa auheni kwa wafanyakazi kufanya kazi zao kwenye jengo hili” alisema Mwinyi
Waziri Mwinyi aliwataka wafanyakzi wa shule hiyo kuhakikisha wanalitunza jengo hilo pamoja na miundo mbinu yake kwa ajili ya vizazi vingine. 
Awali akisoma risala kwa waziri Mwinyi mkuu wa shule hiyo Meja  Erenest Sikaponda alisema kuwa jengo hilo la utawala limejengwa kwa shilingi 222,591,000 na kufanikiwa kuokoa kiasi cha shilingi 103,360,000 kwa kuwa hapo awali BOQ ilikuwa inaonyesha kuwa gharama za jengo ni shilingi 325,951,000.
Kupungua kwa gharama hizo ni kutokana na ubunifu,matumizi mazuri ya rasilimali,nidhamu katika matumizi ya fedha,nguvu kazi ya vijana ambao baadhi yao walikuwa mafundi na gari kubwa la kusombea mchanga,kifusi na mawe msaada huo ulitoka katika kikosi cha 841kj   Mafinga” alisema Maj  Sikaponda
Maj Sikaponda aliwashukuru wadau mbalimbali ambao walitoa msaada wa hali na mali kusaidia ujenzi wa jengo hilo la kisasa la utawala ambalo litakuwa msaada mkubwa kwa wafanyakazi wa shule hiyo.
“Mheshimiwa waziri tunapenda kuwashukuru wadau wafuata TANROAD mkoa wa Iringa kwa msaada wa kifusi cha kujaza msingi kwa trip mia,kampuni ya kichina inayojenga barabara ya Mafinga igawa kwa msaada wa tripu moja ya kokoto ya ujazo wa Mita 15 za mraba,Clement Sangale saruji mifuko 20, na Beruto Kaboda alitoa mbao 2×3 Arobain” alisema Maj Sikaponda
Aidha Maj Sikaponda alisema kuwa jengo hilo la kisasa la utawala linakabili na changamoto ya ukosefu wa samani kutokana na ufinyu wa bajeti hivyo walimuomba waziri kuwasaidia kuzipata samani hizo.
Tumalizie kwa kumshukuru mkuu wa JKT Tanzania pamoja na bodi ya shule kwa usimamizi mzuri wa mipango ya maendeleo ya shule hii.
Kwa upande wake mkuu wa  JKT Tanzania Maj Gen SM Busungu aliwapongeza viongozi waliosimamia ujenzi wa jengo hilo hadi lilipofikia na kuhakikisha linajengwa kwenye ubora unaotakiwa.
Maj Gen SM Busungu alimuomba Waziri wa ulinzi na jeshi la kujenga taifa DR Mwinyi kwenda kuwaombea samani TRA ambazo walizitaifisha kutoka bandarini ambazo maarufu kama samani za makonda ili ziweze kutatua changamoto hiyo katika jengo hilo la utawala. 
Akijibu ombi hilo la mkuu wa Majeshi ya JKT waziri Mwinyi alisema ataenda kuwaomba TRA kwa kuwa wote wanaitumikia serikali moja.

KATIBU MKUU SUSAN MLAWI ATOA MAELEKEZO KWA VIONGOZI WA BODI WA FILAMU.


Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Bi.Susan Mlawi (kulia) akitoa maelekezo na ufafanuzi kwa wajumbe wa Bodi ya Filamu Tanzania kuhusu suala la Sera ya Bodi ya Filamu hatua iliyofikia walipofanya walipomtembelea ofisini kwake leo Jijini Dodoma,kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Filamu Prof.Frowin Nyoni.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Filamu Prof.Frowin Nyoni (katikati) akimweleza Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Bi.Susan Mlawi (wa kwanza kulia)namna uongozi wa bodi hiyo umejipanga kutatua changamoto ya upungufu wa watumishi katika kada mbalimbali ,kushoto ni Mjumbe wa Bodi hiyo Bw.Raymond Kwohelera.
Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Tanzania Bi.Joyce Fissoo akitoa taarifa kwa Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Bi.Susan Mlawi (hayupo pichani) ya kazi za filamu haramu zilizokamatwa mwaka 2016 na kushikiliwa na TRA zenye thamani ya Bilioni 6 kuwa wakati umefika wa kufanyiwa utaratibu stahiki kwa mujibu wa sheria walipomtembelea leo ofisini kwake Jijini Dodoma na baadhi ya wajumbe wa Bodi wa ofisi yake,wa kwanza kulia wajumbe wa Bodi hiyo ambao ni Bw.Raymond Kwohelera na wapili kulia  ni Bi.Anuciatha Leopold.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Bi.Susan Mlawi (wapili kulia)akiwa katika picha ya pamoja baadhi ya Wajumbe wa Bodi ya Filamu Tanzania walipomtembelea ofisini kwake leo Jijini Dodoma,watatu kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Filamu Prof.Frowin Nyoni,na kutoka kushoto watatu ni Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Tanzania Bi.Joyce Fissoo.

KAMANDA SHANNA AONGEZA NGUVU VITA YA UBAKAJI NA VITENDO VYA UKATILI MISUNGWI.



NA ZEPHANIA MANDIA/GSENGOtV

WANAWAKE wilayani Misungwi mkoani Mwanza wameliomba jeshi la polisi kukomesha vitendo vya kinyama dhidi yao ikiwemo kukatwa sehemu za siri na kisha kuuawa ambavyo vimechangia baadhi yao kuishi kwa hofu.
Wakizungumza wakati wa kampeni ya kutokomeza ukatili wa kijinsia wilayani humo, baadhi ya wanawake wamesema kuwa vitendo vya kikatili dhidi yao vimesababisha wengi wao kushindwa kushiriki kikamilifu kwenye shughuli za kujipatia kipato kutokana na hofu ya kuuawa.
Akijibu hoja ya suala la uhakika wa usalama, Kamanda wa polisi mkoa Mwanza JONATHAN SHANA amesema ili kuonesha kuwa Jeshi hilo limedhamedhamiria kuisafisha jamii, tayari mtuhumiwa aliyekuwa akijihusisha na vitendo vya kinyama dhidi ya wanawake na kuwauwa tayari ametiwa mbaroni.
“Mimi kama kamanda wa mkoa wakati yeye anahitimisha mimi nakuja kuzindua kampeni  ya Kupambana na wakatili wa Kijinsia”

“Kama mnavyojua kawaida yangu na kama mlivyokuwa mkiniona mimi nimekuwa nikitoa dakika sifuri tu, pale inapohitimishwa kazi basi mimi ndipo ninapoanza”
“Hivyo nitaanzanao hukuhuku Misungwi”
“Kama wewe umekuwa ukiendeleza ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto, ninapomaliza kuongea hapa, wewe useme Ukatili sasa Basi” Amesema Shanna.

Kampeni ya wiki nane ya kutokomeza ukatili wa kijinsia imeleta matokeo chanya katika wilaya MISUNGWI kufuatia baadhi ya wanaume kuanza kutumia fedha za mauzo ya mazao kwaajili ya maendeleo badala ya matumizi ya anasa. Aidha kampeni hiyo imesaidia kupunguza mimba za utotoni pamoja na utoro.
Kampeni hiyo imetekelezwa na halmashauri ya wilaya hiyo kwa kushirikiana na shirika la kutetea haki za wanawake na wasichana la KIVULINI.
Diwani wa viti maalum tarafa ya inonelwa OLIVER MICHAEL akaliomba jeshi la polisi kukomesha vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake.
Awamu ya kwanza ya Kampeni hiyo imehitimishwa katika kata ya NHUNDULU na mkuu wa wilaya Misungwi JUMA SWEDA


UJENZI WA SEKONDARY HUNGUMALWA NI KASI KASI.



NA ZEPHANIA MANDIA/GSENGOtV

UNAWEZA KUWA NA CHAKULA KINGI LAKINI UKAWA NA NJAA- DKT TIZEBA

Waziri wa kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba akisisitiza jambo leo tarehe 11 Octoba 2018 wakati akizungumza kwenye kongamano maalumu la muelekeo wa siku ya chakula Duniani katika ukumbi wa mihadhara (MLT 9) katika Chuo kikuu cha Sokoine cha Kilimo-SUA Mkoani Morogoro. (Picha Zote Na Mathias Canal, WK)
Waziri wa kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba akisisitiza jambo wakati akizungumza kwenye kongamano maalumu la muelekeo wa siku ya chakula Duniani katika ukumbi wa mihadhara (MLT 9) katika Chuo kikuu cha Sokoine cha Kilimo-SUA, Mkoani Morogoro. Leo tarehe 11 Octoba 2018
Waziri wa kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba (Kushoto) akisalimiana na Mkurugenzi shahada za awali Chuo kikuu cha Sokoine Bi Suzan Agustino wakati alipowasili kushiriki kongamano maalumu la muelekeo wa siku ya chakula Duniani katika ukumbi wa mihadhara (MLT 9) katika Chuo kikuu cha Sokoine cha Kilimo-SUA Mkoani Morogoro. Leo tarehe 11 Octoba 2018
Waziri wa kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba (Kushoto) akikagua Shamba la mafunzo ya Mazao ya kipaumbele (Pamba, Kokoa, Kahawa, Chai, Katani, Miwa na Matunda kabla ya kushiriki kongamano maalumu la muelekeo wa siku ya chakula Duniani katika ukumbi wa mihadhara (MLT 9) katika Chuo kikuu cha Sokoine cha Kilimo-SUA Mkoani Morogoro. Leo tarehe 11 Octoba 2018.

Na Mathias Canal, WK-Morogoro

Utamaduni wa kula aina fulani ya chakula kwa aina moja tu ni miongoni mwa mambo yanayowafanya wananchi kukumbwa na njaa pindi kinapokosekana aina ya chakula kile walichokizoea.

Moja ya matatizo makubwa katika jamii ni pamoja na wananchi kuamini katika utamaduni wa aina moja ya chakula jambo ambalo halipaswi kutiliwa mkazo kwa namna yoyote.

Hayo yamebainishwa na Waziri wa kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba Leo tarehe 11 Octoba 2018 wakati akizungumza kwenye mdahalo wa kuelekea siku ya chakula Dunia ambayo hafla ya kilele chake itafanyika Mjini Tunduma Mkoani Songwe tarehe 16 Octoba 2018.

Katika mdahalo huo ulioandaliwa na Shirika la chakula na kilimo la umoja wa mataifa umoja wa chakula Duniani (FAO), Mpango wa chakula wa umoja wa Mataifa (WFP), Benki ya Kimataifa ya Maendeleo ya kilimo (IFAD) kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine, Waziri Tizeba alisema kuwa katika kipindi hichi Kilimo cha kujikimu sio mjadala serikalini na nchi kwa ujumla bali serikali inaendelea na juhudi za makusudi kusisitiza kilimo cha biashara ili wananchi waondokane na umasikini  wa kipato.

"Na katika hali ya kawaida endapo utekelezaji wa mpango wa kuendeleza sekta ya kilimo awamu ya pili (ASDP II) ukitekelezwa ipasavyo nchi ya Tanzania kabla ya kufikia mwaka 2025 itafikia uchumi wa kati" Alikaririwa Dkt Tizeba na kuongeza kuwa

" Ni lazima tusisitize wakulima kushughulika na kilimo biashara ili waweze kumudu elimu bora, afya bora na kila kitu"

Alisema kuwa njaa haijalishi kile kinachozalishwa bali njaa ni umasikini unaosababishwa na kutokuwa na uwezo wa kupata chakula kwani kuna uwezekana mwananchi asizalishe chakula lakini akawa na uwezo wa kununua chakula chochote anachotaka.

Alisema kuwa serikali imeanza mkakati madhubuti wa kuimarisha masoko ya mazao mbalimbali ndani ya nchi sambamba na kuimarisha masoko ya nje ambapo katika Mpango wa kuendeleza sekta ya kilimo awamu ya pili (ASDP II) muhimili wa tatu ni kuboresha masoko.

“ Ndugu zangu sio kwamba hatuna chakula wakati mwingine chakula kipo lakini watu hawali vizuri kutokana na mila na tamaduni zetu za kiafrika ambapo kwa wakati wote wanawake ndio wapishi na wanaume kusalia kuwa wahemeaji (Kununua).

Kwa upande wake Naibu Makamu wa Mkuu wa Chuo cha Sokoine cha Kilimo (Utawala na Fedha) Prof Yonika Ngaga ametoa pongezi kwa waziri wa kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba kwa kukubali kushiriki mdahalo huo ambao mjadala mkubwa ulihusu kujadili namna bora ya kutatua changamoto ya njaa nchini Tanzania na Barani Afrika kwa ujumla wake.