ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, March 6, 2017

WAKIMBIZI WAANDAMANA NCHINI NIGERIA KULALAMIKIA MAZINGIRA MAGUMU

Wakimbizi wa Nigeria.
WANAWAKE wakimbizi wa Nigeria wamefanya maandamano wakati wawakilishi wa baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa walipokuwa wanatembelea kambi yao ya wakimbizi.
Shirika la habari la Ufaransa limeripoti habari hiyo na kuongeza kuwa, maandamano hayo yamefanyika huko Maiduguri, makao makuu ya jimbo la Borno la kaskazini mwa Nigeria ambalo wakati fulani lilikuwa ni ngome kuu ya genge la Boko Haram.
Waandamanaji hao wamelalamika kwamba mashirika na taasisi zinazosimamia misaada ya kibinadamu zinapora misaada inayotolewa na kusababisha upungufu mkubwa wa chakula kwa wakimbizi hao.
Wajumbe 15 wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wanatembelea nchi nne za Nigeria, Chad, Cameroon na Niger kuangalia hali ya wakimbizi katika nchi hizo za Kiafrika.
Timu hiyo ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ilianza safari yake kwa kutembelea kambi za wakimbizi za nchini Cameroon.

Ramani ya Nigeria.


Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa, lengo la ziara hiyo pamoja na mambo mengine, ni kukusanya taarifa za awali kuhusiana na hali halisi ya mambo nchini Nigeria.
Wananchi wa Nigeria ambao wamelazimika kukimbia makazi yao kutokana na mashambulizi ya genge la kigaidi la Boko Haram, mara nyingi wamekuwa wakiilalamikia serikali ya Nigeria kwa kufanya ufisadi na kupora misaada ya kibinadamu inayotumwa kwa ajili ya wakimbizi.
Kundi la Boko Haram ambalo limetangaza utiifu wake kwa genge la kigaidi la Daesh (ISIS) lilianzisha mashambulizi yake mwaka 2009 nchini Nigeria na mwaka 2015 lilipanua mashambulizi yake hadi katika nchi jirani za Niger, Cameroon na Chad.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.