ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, March 1, 2014

TOTAL YAZINDUA MPANGO WA KUMALIZA TATIZO LA UPATIKANAJI WA UMEME.


Mgeni rasmi, Waziri wa Nishati na Madini, Mh. Prof. Sospeter Muhongo akihutubia wageni waalikwa (hawapo pichani) waliohudhuria katika hafla ya uzinduzi wa bidhaa za AWANGO uliofanyika ndani ya hoteli ya Hyatt Regency, jijini Dar es Salaam, usiku wa jana. Waziri Muhongo aliwapongeza TOTAL kwa juhudi wanazozifanya kusaidia jamii ya Watanzania kupata chanzo cha nishati kitakachowaletea maendeleo ya kijamii na kiuchumi. Pembeni ni baadhi ya bidhaa hizo zinazotumia nishati ya jua
Waziri wa nishati na madini Prof. Sospeter Muhongo (kulia), mgeni rasmi katika hafla ya uzinduzi wa bidhaa zinazotumia nishati ya jua kuzalisha umeme zinazojulikana kama AWANGO, wa kwanza kushoto ni Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania Mh. Marcel Escure pamoja na Mkurugenzi mkuu wa TOTAL nchini Tanzania Bw. Stephane Gay wakishuhudia tukio mojawapo katika hafla hiyo.
Kikundi cha burudani kikionyesha umahiri wa kutoa burudani kwa wageni waalikwa (hawapo pichani) kuashiria uzinduzi rasmi wa AWANGO. AWANGO ni bidhaa zilizo chini ya Mradi wa ‘Total Access to Solar’ ulioanzishwa na kampuni ya TOTAL mwaka 2010 kusaidia kutatua tatizo la upungufu wa nishati kwa nchi zinazoendelea ukiwalenga watu wa kipato cha chini hasa wa vijijini na pembezoni mwa miji.
Meneja wa Maswala ya Kisheria na Ushirika wa kampuni ya TOTAL Tanzania Bi. Marsha Msuya akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya uzinduzi wa bidhaa za AWANGO zilizo chini ya mradi wa TOTAL unaojulikana kama ‘Total Access to Solar’ (TATS) wenye lengo la kutatua tatizo la ukosefu wa umeme nchini Tanzania kwa jamii ya watu wa kipato cha chini. Bi. Marsha alisema kuwa bidhaa hizo zitafika katika mikoa yote nchi nzima.


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
TOTAL YAZINDUA AWANGO KUMALIZA TATIZO LA UPATIKANAJI WA UMEME KWA WATU WA KIPATO CHA CHINI TANZANIA
Dar es salaam, 27 Februari, 2014.
Tatizo la ukosefu wa nishati ya umeme kwa jamii ya watu wa kipato cha chini Tanzania linatarajiwa kufikia kikomo, baada ya TOTAL, moja ya kampuni inayoongoza katika biashara ya nishati duniani, kupitia mradi wa ‘Total Access to Solar (TATS)’ kutambulisha aina mpya ya bidhaa za taa pamoja na vifaa vya kuchajia simu vinavyotumia nishati ya jua vyenye kudumu na vinavyopatikana gharama nafuu nchini Tanzania.   
 
Total Access to Solar (TATS) ni mradi ulioanzishwa na TOTAL mwaka 2010, ukiwa na shabaha ya kuhakikisha upatikanaji wa suluhisho la vifaa vya nishati mbadala katika soko la dunia kwa matumizi ya kijamii na kiuchumi ikilenga jamii ya kipato cha chini.  Mradi wa TATS unaendana na mlengo wa kibiashara wa TOTAL ambao ni “Kuwajibika katika upatikanaji wa nishati kwa watu wengi zaidi kadri inavyowezekana, na kupambana na mahitaji ya dunia”

Miradi ya TATS yote inalenga katika kuleta mabadiliko ya kimaendeleo katika shughuli za kijamii na kiuchumi kwa kutumia nishati itokanayo na vyanzo vya uhakika vikiwemo Jua, Gesi, Mafuta na mabaki ya plastiki. Kwa kugundua mahitaji makubwa ya nishati mbadala kwa Watanzania, TOTAL Tanzania kupitia TATS imezindua rasmi bidhaa mpya zilizo chini ya mradi wa AWANGO, zikiwa ni maalum kwa ajili ya jamii ya Kitanzania.

AWANGO ni mradi unaoleta bidhaa zinazotumia nishati ya jua kuweza kuzalisha umeme. Lengo kuu ni kuwezesha matumizi ya nishati ya jua kama suluhu itakayowezesha upatikanaji wa umeme wa uhakika na nafuu kwa jamii ya watu wa kipato cha chini wanaoishi vijijini na pembezoni mwa miji.

Kabla ya kuzinduliwa Tanzania, mradi wa AWANGO ulishaanza kufanya kazi katika nchi nne duniani huku ukifanyiwa majaribio kwa zaidi ya mwaka mmoja. Baada ya mafanikio katika nchi za Cameroon, Indonesia, Kenya na Jamhuri ya Kongo, zaidi ya taa 125,000 na vifaa vya Jua viliuzwa, baadae mradi huu ulikua na kufikia nchi nyingine nane.

Akihutubia wakati wa uzinduzi wa AWANGO, mgeni rasmi Mhe. Prof. Sospeter Muhongo, ambae ni Waziri wa Nishati na Madini aliwapongeza TOTAL kwa kusaidia kutatua kero ya upatikanaji wa nishati ya uhakika nchini, “kwa niaba ya Serikali, nawapongeza TOTAL kwa kwenda mbali zaidi na kuona uhitaji wa wananchi wetu juu ya mabadiliko na kupiga hatua ya kutatua tatizo upatikanaji wa nishati”.

“TOTAL Wameweza kugundua njia bora ya kuisaidia jamii kwa kuleta vifaa ambavyo vitawasaidia kwenye shughuli za kijamii na kiuchumi. Kama wizara husika tunatambua mchango wa TOTAL kwenye hili na tunawahimiza kuendelea na juhudi zao za kutoa nishati ya gharama nafuu itayopatikana kwa urahisi kwa umma wa Watanzania.” Alisema Prof. Muhongo. 

Kwa kuzingatia mahitaji makubwa ya umeme yanayoongezeka kila siku, bidhaa za AWANGO zimetengenezwa kukabiliana na ongezeko hili. Ufanisi, unafuu na kudumu kwa muda mrefu ndio sababu kubwa zinazofanya ya vifaa vya AWANGO kuwa tofauti na vifaa vingine vilivyozoeleka kutumika na jamii ya kipato cha chini.

Akizungumza juu ya upatikanaji wa bidhaa hizo, Mkurugenzi Mtendaji wa TOTAL Tanzania Bw. Stephane Gay alisema kwamba bidhaa hizi zitapatikana katika vituo vyote vya mafuta vya TOTAL vilivyopo takribani mikoa yote ya Tanzania, lakini pia kampuni hiyo itashirikiana na wadau wa maendeleo zikiwema asasi za kijamii katika usambazaji, ikiwa ni Dhamira ya kupeleka bidhaa za AWANGO nchi nzima.

Ikiwa kama bidhaa ya kibiashara inayosaidia jamii, AWANGO imejidhatiti katika kutoa huduma bora na ufanisi mkubwa kama ilivyo TOTAL. Mradi huu unatazamiwa kuwa na matokeo matatu katika njia tofauti za Kiuchumi, kijamii na kulinda mazingira. Shabaha kubwa ni kumpa Mwananchi wa kipato cha chini nguvu ya kujikwamia kimaendeleo kijamii na kiuchumi.

KUHUSU TOTAL
TOTAL Tanzania Ltd ni kampuni inayojishughulisha na usambazaji wa bidhaa za nishati ya petroli na mafuta ghafi. Kampuni hiyo ilianzishwa mwaka 1969 ikiwa na makao makuu yake Dar Es Salaam, Tanzania

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.