ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, July 4, 2017

AMIRI KILAGALILA STORY SHULENI KAMBARAGE.

Jumla ya Tsh 450,000 zimetolewa na Mbunge wa viti maalumu kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA mkoa wa Njombe Lucia Mlowe ikiwa ni sehemu ya kuchangia ujenzi unaoendelea katika shule ya msingi Kambarage.


Hatua hiyo imekuja ikiwa ni utekelezaji wa ahadi aliyoitoa mbunge huyo mwezi machi mwaka huu katika harakati za kuhamasisha ujenzi wa shule ya msingi kambarage iliyopo katika halmashauri ya mji wa Njombe.


Taarifa NA:AMIRI KILAGALILA


Akimwakilisha mbunge Lucia Mlowe, katibu wa mbunge huyo Bw.Semeni Deusi Msigwa amesema kiasi hicho cha fedha ni kwaajili ya kuchangia mifuko ya saruji 26  pamoja na milango miwili katika kufanikisha ujenzi unaoendelea shuleni hapo.


CUE….SEMENI MSIGWA


Pamoja na kutoa shukrani  mkuu wa shule ya msingi Kambarega Jeni Resmu ng’umbi  amewataka viongozi wengine kuendelea kuchangia ili kukamilisha ujenzi wa shule hiyo.


CUE…JENI NG’UMBI


Kwa upande wake mtendaji wa mtaa wa Kambarage Bw,izack mwakyusa pamoja na mambo mengine amesema mchango huwa dira ya kulisukuma mbele gurudumu la maendeleo katika mtaa huo.


CUE…. IZACK MWAKYUSA

Shule ya msingi kambarage inajumla ya wanafunzi 1206 na kati yao 26 ni wanafunzi wenye mahitaji maalumu wakiwemo wenye mtindio wa ubongo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.