ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, June 12, 2017

MCHANGA WA MAGUFULI WAMCHOMOA TABASAMU CHADEMA, ASEMA SASA BASI YUKO TAYARI KUJIUNGA NA CHAMA CHOCHOTE SIYO CDM

Baada ya kusomwa Ripoti ya kamati ya pili kuhusu mchanga wa madini huku ikiwaibua Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge na Mbunge wa Sengerema, Wiliam Ngeleja kuhusu mikataba ya madini iliyoingiwa miaka iliyopita.

Mmoja wa wanachama wa CDM aliyekuwa mpinzani wa Ngeleja kwenye uchaguzi uliopita maarufu TABASAMU amebadili msimamo wake na hata kuamua kujivua uanachama na sasa anafikiria chama atakachojiunga nacho.


 Zaidi sikiliza KAZI NA NGOMA YA JEMBE FM SIKU YA JUMANNE YA TAREHE 13 JUNE 2017 SAA 5 HADI 7 MCHANA

KOMENTI ZA WADAU ITANDAONI:-
They knew what they were doing. Mkapa alizawadiwa bonge la dhahabu na Barrick. Kikwete alijisifia kwenye hotuba yake Indaba 2007 Afrika kusini jinsi alivyokata mbuga kuwaleta wachimba madini. They knew what they were doing.
 

Wanasiasa wengi ni uchwara, wapo wapo tu kupiga kelele na ngonjera! we are just not serious ! Unawezaje kumuacha waziri wa madini aliekuwepo JK ? Unawezaje kumuacha BWM ? katika hili ? Hao wametutafuna sana ila mnawashangilia kama zuzu !

Nimesikiliza report ya pili iliyosomwa hivi punde na nimekumbuka busara za mwalimu kwamba hatukuwa tayari kuchimba madini. Kinachoonekana ni kana kwamba viongozi wetu walikuwa au hawaelewi wanachosaini au rushwa iliwapofusha macho.

 J........... huoni VIROBOTO wameshaanza KAZI ya kutetea.. mara oooh walikuwa hawaelewi wanachosaini....!!!

Rwebu! Tunapaswa kuwa tayari kusikiliza hata mawazo ambayo hatuyapendi.


Mkuryamstaarabu.......Mchanga wa madini haujawahi kumwacha MTU salama.

AyoubDalushi Tupo pamoja tunamwombea rais wetu.

Kuhusu kwamba hawakufahamu siyo kweli kabisa.

Labda nikuulize wewe je ni mara ya kwanza kusikia haya?

This is typical CSO songs and dance for the past decade and more, What is new in this anyway?

Au ni mpya kwa vile ni mwiko kwenu kusikiliza mawazo ya upande wa pili. Au upya wake labda kwa vile mmesema nyie.


King_roy-assenga Kweli hii ilikuwa sehemu ya kuchua Tanzania ya watu mambumbumbu kweli kwa sasa rais wetu hana toa watu ambao walikuwa wanapewa majukumu ya kuwasaidia watanzania wanajisaidia kweli.

Kwangu mimi hakuna ninachoshangaa chochote; viongozi wetu, akiwamo mukulu mwenywewe waliyajua yote haya. Nangoja sasa tuletewe na taarifa mahsusi kuhusu EPA, Lugumi, Meremereta, Escrow, you name it; zote ni dizaini hiyo hiyo!

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.