ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, May 28, 2017

YANGA YATALII VYEMA JIJI LA ARUSHA YASHUSHA KICHAPO KWA AFC NA JEH WAJUA NINI SABABU ZA KUPOROMOKA KWA SOKA LA MKOA HUO


NA ALBERT GSENGO: ARUSHA
Mabingwa wa Vodacom Premier League Dar es salaam Young African leo wameshusha kichapo cha mabao ma 3-0 kwa timu ya AFC iliyo kuwa ikicheza nyumbani kwake dimba la Sheik Amri Abeid mjini Arusha, katika mchezo wa kirafiki wa kusherehekea ushindi na kulionesha kombe kwa mashabiki wake, baada ya timu hiyo ya mtaa wa Jangwani mwishoni mwa juma lililopita kutawazwa mabingwa wa VPL msimu wa 2016-2017 Tanzania Bara.

Wakicheza mbele ya maelfu ya mashabiki waliojitokeza kwa wingi mjini Arusha, Yanga walifungua karamu yao kwa goli la kwanza lililofungwa na Jofrey Mwashuiya kunako dakika ya 23, kisha baadaye mchezaji huyo huyo alirudi kubisha hodi tena langoni mwa AFC na kufunguliwa kunako dakika ya 67 kipindi cha pili..

Samwel Greyson aliyeingia badala ya Emmanuel Martin aliyeenda benchi aliizawadia Yanga bao la 3 na la ushindi ikiwa ni dakika 4 kabla ya filimbi ya mwisho ya mchezo kulia.

Mara baada ya mchezo Jembe Fm inazungumza na makocha wa timu zote mbili BOFYA PLAY KUMSIKILIZA MWAMBUSI.
Fikiri Elias ni mwalimu wa AFC ya Arusha naye alifunguka hivi:- BOFYA PLAY KUMSIKIA

Mashabiki dimbani Sheik Amri Abeid mjini Arusha AFC  v/s Yanga.
Patashika ...
Zipo changamoto ambazo zinashabihiana na zile zinalo liandama soka la Mwanza.
Lakini jeh wajua nini sababu ya soka la Arusha kuporomoka? Mwakilishi wetu Albert G Sengo alikuwa mjini humo naye hapa anazungumza na Kocha wa zamani wa AFC, kwanza tahimini kisha nini sababu ya soka kuporomoka. BOFYA PLAY KUSIKIA










Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.