ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, April 3, 2017

WATU WENYE SILAHA WAWAFYATULIA RISASI RAIA WAKIWA SOKONI NCHINI SUDANI, SABA WAUAWA.


WATU wenye silaha wasiojulikana wametekeleza shambulizi katika soko nchini Sudan na kuua watu saba na wengine kadhaa kujeruhiwa.
Habari nchini humo zinaarifu kuwa, tukio hilo lilitokea Jumapili ya jana huko katika jimbo la Kordofan magharibi ambapo watu wenye silaha wasiojulikana wakitumia magari ya kiraia walishuka kutoka katika magari hayo na kuanza kuwafyatulia risasi watu waliokuwa sokoni. Hadi sasa hakuna kundi lililotangaza kuhusika na hujuma hiyo.

Rais Omar al-Bashir wa Sudan
Inafaa kuashiria kuwa, waasi wa majimbo ya Kordofan kusini na Blue Nile wanapambana na jeshi la serikali ya Khartoum tangu mwaka 2011. Mapigano huko Darfur, yalianza mwaka 2003 baada ya makabila ya eneo hilo kuituhumu serikali ya Rais Omar al-Bashir wa Sudan kwa kufanya ubaguzi dhidi yao. Ripoti iliyotolewa na Umoja wa Mataifa imetangaza kuwa, katika mapigano yaliyojiri maeneo ya machafuko nchini humo, karibu watu laki tatu waliuawa Darfur na zaidi ya wengine milioni mbili na laki tano kuwa wakimbizi.


Madhara ya siulaha za kemikali zinazotajwa kutumiwa na jeshi la serikali dhidi ya raia
Kwa kawaida raia wa kawaida ndio huwa wahanga wa mashambulizi ya waasi na askari wa serikali. Mwanzoni mwa mwezi Machi uliomalizika shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International lilitoa wito wa kufanyika uchunguzi kuhusu mashambulizi ya silaha za kemikali yaliyofanywa na serikali ya Sudan dhidi ya raia wa kawaida katika eneo la Darful, magharibi mwa nchi hiyo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.