ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, January 21, 2017

TRUMP AANZA KUFANYIA MABADILIKO SHERIA ZA OBAMA.

The inaugural parade passing by President Donald J. Trump at Lafayette Park, near the White House, on Friday.
U.S. President Donald Trump waves to supporters as he walks the parade route with his wife, Melania, after being sworn in on Friday.
Trump na mkewe wakitembea mjini Washington


Rais wa Marekani Donald Trump ameanza kutia saini maagizo ya rais, baadhi yake yakiwa ni ya kubadili yale yalioafikiwa na mtangulizi wake Barak Obama.

Muda mfupi baada ya kukagua gwaride la kuapishwa kwake, Bw Trump, alitia amri ya serikali, kupunguza mzigo wa kiuchumi kwa taifa, unaotokana na gharama za kufadhili bima ya matibabu ya bei nafuu inayofahamika kama Obamacare, ambayo Trump aliahidi kufanyia marekebisho.

693719551KE00014_Parade_Cel
A military band marches during the inaugural parade. Trump ni rais wa 45th wa The United States. (Joe Readle/Getty Images)

Trump pia ametia saini amri ya kuwaidhinisha mawaziri wake wapya wa Ulinzi na usalama wa kitaifa ambao uteuzi wao umepitishwa na bunge la seneti.


Utawala wa Trump pia umeaanza kufanyia marekebisho mtandao wa kijamii wa Ikulu ya White House kwa kuweka masuala yatakayopatiwa kipaumbele na uongozi huo mpya.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.