ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, September 7, 2016

DC WA HANDENI GODWIN GONDWE ASULUHUSHA MGOGORO WA MPAKA ULIODUMU KWA MUDA MREFU

 Mkuu wa wilaya ya Handeni wa kwanzakushoto  akisoma ramani ya mwaka 2007 akiwa na  viongozi na wananchi ili kujua mpaka upo sehemu gani.DC Gondwe  amefanikiwa kusuluhisha mgogoro wa mpaka uliodumu kwa muda mrefu akiwa ameambatana na Wakurugenzi wa halmashauri zote mbili uliohusisha Kijiji cha Kweditilibe cha Handeni vijijini na kitongoji cha makinda kilichopo Handeni Mji.

RAMANI YA 2007  ndiyo iliyotumika kusuluhisha mgogoro huo ambapo aliwaeleza wananchi kuwa ramani hiyo ndiyo iliyotumika kuweka mipaka ya maeneo husika Tanzania nzima na hakuna mwenye mamalaka ya kuibadili isipokua Raisi mwenye mamalaka ya Ardhi ya Tanzania nzima.
Mkuu wa wilaya Mh. Godwin Gondwe akisalimiana na mmoja wa wananchi wa Wilaya ya Handeni kabla ya zoezi la kutatua mgogoro wa mpaka.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.