ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, March 14, 2016

MTOTO AUAWA KWA MPINI WA JEMBE.


Polisi mkoani Mwanza inawashikilia watu wawili kwa tuhuma za mauaji yakiwamo ya mtoto wa miaka sita kwa kupigwa na mpini wa jembe kichwani.
Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Justus Kamugisha alisema kuwa mkazi wa Gulumungu wilayani Misungwi anashikiliwa kwa tuhuma za mauaji ya mtoto huyo, Zawadi Shija (6).
Kamugisha alisema mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo kama njia ya kumkomoa bibi wa mtoto huyo, Samaka Mashala ambaye wanagombea mpaka wa shamba.
Alisema tukio hilo lililozua simanzi miongoni mwa wakazi wa kijiji hicho lilitokea Machi 9.
Alisema kabla ya kuuawa, Zawadi alitumwa dukani na dada zake, lakini alichelewa kurejea nyumbani hali iliyosababisha aingiwe hofu ya kuadhibiwa na kuamua kujibanza nyuma ya nyumba ya jirani yao.
“Yule jirani alipomuona mtoto yule amejibanza nyuma ya nyumba, alihamaki na kuanza kumshambulia kwa mpini wa jembe na kumsababishia majeraha makubwa yaliyosababisha kifo chake wakati anapatiwa matibabu Kituo cha Afya Misasi,” alisema.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.