ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, October 26, 2014

YANGA ILIVYO ICHACHAFYA STAND UNITED DIMBA LA CCM KAMBARAGE JANA.

Kikosi cha Stand United.
BOFYA PLAY KUSIKILIZA YALIYOJIRI.
Yanga.
Mbunge wa Shinyanga mjini Mhe. Stephan Masele akisalimia na mchezaji wa Yanga Jaja wakati wa utambulisho kabla ya mchezo dhidi ya Stand United uliochezwa dimba la CCM Kambarege mjini Shinyanga. Hadi mwisho wa mchezo Stand United ilikubali kichapo cha bao 3-0.
Mbunge wa Shinyanga mjini Mhe. Stephan Masele akisalimia na beki wa Yanga Yondani wakati wa utambulisho kabla ya mchezo dhidi ya Stand United uliochezwa dimba la CCM Kambarege mjini Shinyanga. Hadi mwisho wa mchezo Stand United ilikubali kichapo cha bao 3-0.
Mbunge wa Shinyanga mjini Mhe. Stephan Masele akisalimia na wachezaji wa Stendi United kabla ya mchezo dhidi ya Yanga uliochezwa dimba la CCM Kambarege mjini Shinyanga. Hadi mwisho wa mchezo Stand United ilikubali kichapo cha bao 3-0.
Mbunge wa Shinyanga mjini Mhe. Stephan Masele akisalimia na wachezaji wa Stendi United kabla ya mchezo dhidi ya Yanga uliochezwa dimba la CCM Kambarege mjini Shinyanga. Hadi mwisho wa mchezo Stand United ilikubali kichapo cha bao 3-0.
Nani kuanza mchezo.
Urushaji wa Mbuyu Twite ni kama kona vile.
 Mara baada ya kumalizika dakika 45 za kipindi cha kwanza timu zikienda mapumziko na Yanga ikiongoza kwa goli moja kulitokea vurugu baina ya Kocha wa Yanga na wachezaji wake dhidi ya mashabiki na viongozi wa Stand United ambapo Yanga walikuwa wakishinikiza kwenda vyumba vya mikutano jukwaa kuu wakigomea kwenda katika vyumba vya kawaida vya mapumziko. 
Vurugu zilikolea mara baada ya wachezaji wa Yanga wakiongozwa na kocha wao Marxio Maximo kupanda jukwaa kuu wakidai kuwa vyumba vya kubadilishia nguo vilivyoko uwanjani ni vichafu wakihitaji kutumia vyumba vilivyoko jukwaa kuu , kitendo ambacho kilipingwa na mashabikiwa Stand united na kuanza kuwarushia chupa za maji na kuwazomea.


 Pichani wachezaji wa Yanga wakiwa jukwaani na kocha wao. Wachezaji hao walisikika wakisema vyumba vilivyopo uwanjani hapo ni vichafu.
Hapo ndipo vurugu zikaanza,wachezaji wa Yanga kukabiliana na mashabiki wa Stand United, polisi wakiamua makonde yakirushwa, chupa za maji zikirushwa hovyo.
Dakika ya 79 Yanga wanapata bao la pili kupitia Jeryson Tegete aliyeingia kuchukuwa nafasi ya Jaja. 
Dakika ya 90 Wachezaji wa Yanga wanasherehekea goli la tatu mfungaji ni yuleyule Jerson Tegete. 
Hivi ndivyo vyumba vya kubadilishia nguo ambavyo timu ya Yanga waligoma kuingia kipindi cha pili.
Mazingira ya ndani ya vyumba hivyo.
Mashabiki wa Yanga wakipongezana mara baada  ya ushindi dhidi ya Stand United 3-0. 
3-0 toka uwanja wa CCM Kambarage mjini Shinyanga.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.