ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, September 14, 2012

MUINGEREZA AKAMATWA UGANDA KWA USHOGA

David Cecil katika mahakama ya Makindye

Msanii moja toka Uingereza amekamatwa nchini Uganda kwa madia ya kuandaa na kuonyesha mchezo wa kuigiza kuhusu ushuga.
Mtayarishi David Cecil wa Uingereza alifikishwa katika mahakama moja mjini Kampala na kushitakiwa kwa madia ya kukaidi na kupuuza amri ya serikali. Polisi wanasema kuwa Muingereza huyo alionyesha mchezo huo wa kuigiza licha ya kwamba Uganda ilipiga marufuku kwa muda onyesho hilo.
Mahakama hiyo iliambiwa kuwa Bwana Cecil alionyesha mchezo huo kwa jina "The river and the mountain" katika ukumbi wa Tilapia Cultural Center taraehe 17 Agosti na pia katika ukumbi mwengine wa Mish Mash Cultural Center tarehe 26 Agosti mjini Kampala.
Mahakama hiyo ya Kampala ilikataa kuamuachilia Muingereza huyo kwa dhamana na badala yake kuagiza awekwe katika gereza la Luzira hadi siku ya jumatatu ,Septemba 17 ambapo kesi yake inatarajiwa kuendelea.
CHANZO: BBC Swahili.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.