ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, September 13, 2012

MADIWANI WALIOVULIWA UANACHAMA CHADEMA WATOA TAMKO

DIWANI wa Kata ya Kitangili Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza Henry Matata na Diwani  wa Kata ya Igoma Halmashauri ya Jiji la Mwanza (Nyamagana) Adam Chagulani wote kutoka Chama cha CHADEMA wametoa tamko lao kwa vyombo vya habari leo kupinga maamuzi ya Kamati kuu ya Chama hicho ya kuwavua uanachama hivi karibuni kwa madai ya kukisaliti chama na kula njama kukushinikiza kumung’oa aliyekuwa Meya wa Jiji la Mwanza Josephat Manyerere (Nyakato).


Diwani wa kata ya Kitangili Henry Matata.

Diwani Matata (Kitangili) alisema kwamba kikao cha kamati kuu kilichoketi mwishoni mwa juma lililopita na kutoa uamuzi huo Jijini Dar es salaam kiligubikwa na ushabiki na pia ukiukwaji wa Katiba ya Chama hicho na ile ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hivyo wameamua kwenda mahakamani kufungua kesi ya kuzuia uamuzi huo wa Kamati kuu ya CHADEMA wa kuwavua uanachama ili kukosa madaraka (Udiwani)  ikiwa wao walichaguliwa na wananchi zaidi ya elfu nne.

Akifafanua Matata amedai kuwa moja ya sababu kubwa zilizowafanya kukimbilia mahakamani yeye na diwani mwenzake Chagulani ni kutaka haki itendeke kwa vile madai na tuhuma zilizotolewa dhidi yake ni za uongo ambazo hazina ukweli bali kwa shinikizo la wabunge wa chama hicho wa majimbo ya Ilemela, Nyamagana na Ukerewe kutokana na kuwepo kutokuelewana baina yao na madiwani hao wanaodaiwa kuwahofia kisiasa.

Diwani wa Igoma Adam Chagulani.
 Kwa upande wake Chagulani (Igoma) alieleza kuwa hatua hiyo imetokana na Kamati kuu ya chama hicho Taifa kukubaliana na mapendekezo yaliyotolewa na baadhi ya viongozi ambao wamekuwa akishirikiana na wabunge wa Chama hicho wa Majimbo ya Ilemela Haghiness Kiwia na Ezekia Wenje Nyamagana kutokana na wao kutofautiana nao kwenye vikao vya baraza la madiwani na vya chama wakati wa kuchangia hoja kwa lengo la kuwatumikia wananchi waliowachagua.

Chagulani alisema kwamba umefika wakati wa viongozi wa chama hicho kuacha kutumia ubabe wa kuamua kuwafukuza wawakirishi wa wananchi waliochaguliwa kwa kisingizio cha kukisaliti chama hicho bali watambue kuwa wao ni kiungo cha kuwatumikia wananchi na kuwawakilisha kwenye mabaraza ili kuzitafutia kero zao ufumbuzi na CHADEMA lazima itumie vikao vya chini na kuifuata vyema Katiba yake na hatua za wenye makosa kujadiliwa kuanzia ngazi ya kata, wilaya, mkoa na Taifa badala ya kuanzia juu kisha kutoa uamuzi hiyo si demokrasia hata kidogo bali ni udikiteta wa demokrasia ndani ya vyama vya siasa.

BARUA ALIYOANDILIWA MH. DIWANI CHAGULANI KUVULIWA UANACHAMA CHADEMA


Diwani wa Kata ya Kitangili Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza Henry Matata (kushoto) na Diwani  wa Kata ya Igoma Halmashauri ya Jiji la Mwanza (Nyamagana) Adam Chagulani wote kutoka Chama cha CHADEMA wakizungumza na vyombo vya habari kutoa tamko lao kupinga maamuzi ya Kamati kuu ya Chama hicho ya kuwavua uanachama.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.