ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, January 19, 2018

NEW ZEALAND: WAZIRI MKUU AFUNGUKA KUWA NA UJAUZITO


Waziri mkuu wa New Zealand mwenye umri wa miaka 37 Jacinda Ardern amefichua kwamba yeye ni mjamzito.

Bi Ardern alisema kwamba yeye na mpenzi wake Clarker Gayford walikuwa wakitarajia mwana wao mwezi Juni ambapo baadaye atachukua likizo ya wiki sita.

''Na tulidhani kwamba mwaka 2017 ni mwaka mkuu'', aliandika katika mtandao wake wa Instagram.

Bi Ardern mwenye umri wa miaka 37 alikuwa waziri mkuu mwenye umri mdogo nchini New Zealand tangu 1856 akiungwa mkono wakati alipotangaza kuhusu hali yake mpya siku ya Ijumaa.

Chama cha leba cha Bi Ardern kilikuwa cha pili katika uchaguzi wa mwezi Septemba ambapo hakuna chama kilichofanikiwa kupata wingi wa kura.

Aliunda serikali kupitia usaidizi wa Winston Peters ambaye ni kiongozi wa chama kidogo cha New Zealand.

''Nitakapokuwa ugenini Bwana Peters atakuwa kaimu waziri mkuu, akifanya kazi na ofisi yangu mbali na kuwasiliana nami'', alisema bi Ardern katika taarifa ilioripotiwa na gazeti la New Zealand Herald siku ya Ijumaa.

''Nitawasiliana na kupatikana katika kipindi hicho cha wiki sita wakati nitakapohitajika''.

Bi Ardern alisema kuwa aligundua kwamba ni mjamzito siku sita kabla ya kujua kwamba atakuwa waziri mkuu , na lilikuwa swala la kushangaza.

''Mimi sio mwanamke wa kwanza kufanya kazi mbili.Sio mwanamke wa kwanza kufanya kazi huku nikihudumia mwanangu, kuna wanawake wengi ambao wamekuwa katika hali kama hii awali'', alisema.

''Bwana Gayford atakuwa baba ambaye atakuwa akisalia nyumbani'', aliongezea.

Mawaziri 2 wakuu wa zamani nchini humo walikuwa watu wa kwanza kutoa pongezi zao.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.