ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, June 20, 2017

NYOTA WA TOTTENHAM HOTSURS VICTOR WANYAMA AZURU TANZANIA.

Victor Wanyama amesema zaidi anazijua Yanga, Simba na Azam FC linapozungumziwa soka nchini.

Kiungo huyo nyota wa Tottenham Hotspurs ya England ametua nchini akiongozana na ndugu zake.

Wanyama yuko nchini kwa mapumziko na amesema anajua soka ya Tanzania, sawa na Kenya lakini timu hizo tatu ndizo anazozijua zaidi.

"Nazijua Yanga, Simba pia Azam FC. Soka la Kenya na Tanzania hakuna tofauti kubwa.

"Watu wa Afrika Mashariki tunapaswa kuungana na kusaidia maendeleo kwa ujumla," alisema Wanyama.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.