ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, April 25, 2017

MBAO YAPANIA KUICHARAZA YANGA FA.

MBAO YAPANIA  KUICHARAZA YANGA FA


NA ANNASTAZIA MAGINGA,Mwanza

UONGOZI  wa Timu ya mbao fc usema  wamejipanga kuhakikisha timu yao inaibuka na ushindi katika mchezo wa nusu fainali wa kombe la FA dhidi ya Yanga  unaotarajiwa  kuchezwa  hivi karibuni kwenye uwanja wa CCM kirumba jijni hapa.


Mbao fc imeingia katika hatua hiyo baada ya kuitupa  nje Kagera sugar kwa bao 2-1katika uwanja wa Kaitaba mkoani Kagera huku Yanga ikitinga hatu hiyo kwa kuifunga Prisons bao 3-0 katika mchezo wa robo fainali uliochezwa uwanja wa Taifa Dar es Salaam.


Ofisa habari wa Mbao fc Chrisant Malinzi ameiambia G sengo blog kuwa uongozi wa timu hiyo umejipanga vizuri kuhakikisha kikosi cha chake kinaibuka na ushindi katika mchezo huo ili kutinga katika hatua ya fainali na kutwaa taji la kombe hilo.

“Hatutegemei kupoteza mchezo huo kwani tumejipanga kufanya vizuri ili kutimiza malengo yetu ya kucheza fainali kwa mara ya kwanza na kutwaa ubingwa wa kombe la FA” amesema Malinzi


Ameeleza kuwa wamejipanga na kwamba hawana  hofu yeyote na mchezo wa nusu fainali ya kombe la FA dhidi ya Yanga utakaofanyika kwenye uwanja waon wa Nyumbani CCM kirumba  ili kutimiza malengo .

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.