ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, April 13, 2017

WATANZANIA 8 WALIOKABILIWA NA KESI YA UJASUSI, WAACHILIWA MALAWI.

WATANZANIA wanane waliokuwa wanakabiliwa na kesi ya ujasusi, nchini Malawi wameachiwa huru jana na sasa wapo njiani kurejea nchini Tanzania .

Hukumu ya kesi yao ilitolewa jana jioni tarehe 12 mwezi Aprili mwaka huu,Watanzania hao waliokuwa wanashikiliwa katika Gereza Kuu la Mzuzu nchini Malawi kwa tuhuma za kuingia kinyume cha sheria katika mgodi wa urani uliopo eneo liitwalo Kayerekera.

Serikali ya Tanzania ilikataa kwamba Watanzania hao walitumwa na serikali ili kufanya shughuli za kijasusi katika mgodi huo wa urani. Tanzania iliongeza kwamba watu hao walikuwa ni wafanyakazi wa Taasisi ya misaada ya Caritas iliyo chini ya Kanisa Katoliki Jimbo la Songea mkoani Ruvuma.

Wakili aliyekuwa anaisimamia kesi hiyo ,Flaviana Charles ameiambia BBC kuwa watu hao kwa sasa wako huru pamoja na kuwa wamepitia katika magumu mengi na ya kukatisha tamaa lakini kila kitu kilikuwa wazi na upande wa walalamikaji hawakuwa na ushaidi wa kutosha wa kuwafunga kwa kuwa watanzania hao waliingia nchini humo kihalali kuanzia mpakani na walikuwa na mualiko na wakati wanawakamata walikuwa hawajafika mgodini bado maana walikamatwa wakiwa wanatoka hotelini hivyo hawakufika mgodini au kuhoji mtu yeyote hivyo shutuma zao zilikuwa zenye mashaka sana.

Je,kuna fidia ambayo wamelipwa baada ya kuwekwa kizuzini tangu mwezi desemba mwaka jana?
Wakili Flaviana amesema kuwa kuna ujanja ambao mahakama imeutumia ili kukwepa fidia kwa kudai kuwa ambayo wameshatumikia kifungo kwa kipindi hicho chote watuhumiwa hao walipokuwa kizuizini hivyo kwa sasa wako huru.

BBC imezungumza pia na baadhi ya watu hao waliokuwa wanatuhumiwa,,wanasema wana furaha sana maana walikuwa wameenda Malawi kwa matarajio ya kukaaa siku 3 lakini sasa wamejikuta wamekaa zaidi ya miezi mitatu,bila kujua kinachoendelea katika familia zao pamoja na shughuli zao za kila siku

wamesema walikuwa wakiteseka bila sababu ilhali nia yao kwenda Malawi ilikuwa njema kabisa .
Watanzania hao nane,wanashukuru sana serikali yao ya Tanzania haswa kwa balozi kufika kuwaona.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.