ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, December 11, 2016

HAWA HAPA WASHINDI WA EATV AWARDS 2016


Mwanamuziki Ali Kiba akipokea tuzo yake ya ushindiwa Wimbo Bora wa Mwaka kutoka kwa Nandi Mwiyombela kutoka kampuni ya Vodaco Tanzania katika Tuzo za Muziki za EATV AWARDS zinazofanyika usiku huu kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam. 
PICHA ZOTE NA SUFIANI MAFOTO.


Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akikabidhi Tuzo ya Heshima kwa DJ Boniventura Kilosa aka Bony Love baada ya kutangazwa mshindi wa heshima katika tuzo za EATV AWARDS 2016 zilizofanyika usiku huu kwenye ukumbi wa Malimani City jijini Dar es salaam. 


Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya, Lady Jay Dee akipongezwa na Mpenzi wake mara baada ya kupokea tuzo yake katika hafla ya utoaji wa tuzo za EATV AWARDS zilizofanyika kwenye ukumbi wa Malimani City jijini Dar es salaam jana usiku.
 




DJ Boniventura Kilosa aka Bony Love akipongezwa na DJ John Dilinga mara baada ya kupokea tuzo yake ya Heshima katika tuzo zilizoandaliwa na Kituo cha Televisheni cha EATV.

Waziri wa Habari, Utamaduni ,Sanaa na Michezo Mh. Nape Nnauye akiwa katika picha ya pamoja na Wasanii mbalimbali waliojinyakulia tuzo zao usiku wa leo.

Historia imeandikwa kwenye tasnia ya sanaa nchini ambapo kwa mara ya kwanza tukio la utoaji wa tuzo za #EATVAwards kwa wasanii wa muziki na filamu Afrika Mashariki, limefanyika usiku wa leo katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam.
Tuzo hizo zilizoandaliwa na East Africa Television Ltd, zimekuwa za kwanza Afrika Mashariki, ambapo wasanii mbali mbali wamefanikiwa kujinyakulia tuzo zao.

Tazama orodha nzima ya washindi hapa chini..

Kipengele cha mwanamuziki bora wa kiume
G Nako – 'Original'
Sheta –'Namjua'
Mwana FA – 'Ahsanteni kwa Kuja'
Alikiba – 'Aje' --- MSHINDI
Ben Pol – 'Moyo Mashine'

Mwana muziki bora wa kike
Lilian Mbabazi – 'Yoola'
Ruby – 'Forever'
Lady Jay dee – 'Ndindindi' --- MSHINDI
Linah – 'No stress'
Vanessa Mdee – 'Niroge'

Mwanamuziki bora chipukizi
Manfongo – 'Hainaga ushemeji' --- MSHINDI
Feza Kessy – 'Sanuka'
Rukia Jumbe (Ruky Baby) – 'Mpasuo'
Bright – 'Nitunzie'
Mayunga – 'Nice couple'

Kundi bora la mwaka
Navy kenzo – 'Kamatia chini'--- MSHINDI
Mashauzi Clasic - 'Kismat'
Team Mistari – 'Tuzidi'
Sauti Sol – 'Unconditional bae'
Wakali wao – 'Chozi langu utalilipa'

Video bora ya mwaka
Njogereza – Navio
Namjua – Shetta
Aje – Alikiba -- MSHINDI
Don't Bother – Joh Makini
Ndindindi – Lady Jaydee

Wimbo bora wa mwaka

Don't bother – Joh Makini
Ndindindi - Lady Jayedee
Kamatia chini - Navy Kenzo
Moyo mashine – Ben Pol
Aje – Alikiba --- MSHINDI

Filamu bora ya mwaka
Facebook profile
Safari ya Gwalu --- MSHINDI
Mfadhili wangu
Hii ni laana
Nimekosea wapi

Muigizaji bora wa kiume

Meya Shabani Khamisi
Salim Ahmed (Gabo) --- MSHINDI
Daudi Machael (Duma)
Doto Hussein Matotola
Said Mkukila

Muigizaji bora wa kike

Chuchu Hansy --- MSHINDI
Rachel Bithulo
Frida Kajala Masanja
Khadija Ally

TUZO YA HESHIMA

DJ Maarufu bongo Boniventure Kilossa (Dj Bonny Love) ndiye mtu aliyepewa tuzo maalum ya heshima, akitambuliwa kutokana na mchango wake kwenye tasnia ya sanaa hapa nchini

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.