ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, October 19, 2016

JELA KWA KUGHUSHI HUDUMA ZA NHIF.

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Kinondoni imewahukumu wakazi wawili wa Mkoa wa Dar es Salaam kifungo cha miaka miwili jela au faini ya shilingi Milioni moja kwa makosa ya kujipatia huduma za Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya kwa njia za udanganyifu.
Hukumu hiyo imetolewa leo mahakamani hapo na Hakimu Mkazi Mwandamizi Bweguge Obadia ambaye alisema kuwa ushahidi uliotolewa na mashahidi wa upande wa mashitaka umeithibitishia mahakama pasipo shaka ya aina yoyote kuwa washitakiwa hao walitenda makosa hayo.

Waliohukumiwa kifungo hicho ni pamoja na Bw. Michael Francis na Bw. Godfrey Nyika ambao ni washitakiwa wa pili na wa tatu huku mshitakiwa wa kwanza Bw. Rashid Kidumule akiaachiwa huru baada ya kuthibitika kutotenda kosa hilo.

Akisoma hukumu hiyo Hakimu Mkazi Mwandamizi Bw. Obadia alisema kuwa hakuna shaka yoyote juu ya washitakiwa hao kutenda makosa ya kujiwakilisha katika duka la dawa la Nakiete kwa lengo la kujipatia huduma ya dawa kwa kutumia kitambulisho cha matibabu cha mshitakiwa wa tatu ambaye ni Bw. Nyika.

“Ushahidi wa mashahidi wa mashitaka unathibitisha bila kuacha shaka yoyote kuwa mshitakiwa wa pili Bw. Francis alijiwakilisha dukani kwa lengo la kupata dawa kwa kutumia kadi isiyo yakwake na hakuna shaka kuwa mshitakiwa wa tatu ambaye ndiye mwenye kadi alimpatia kadi hiyo mshitakiwa wa pili hivyo kwa ushahidi huu Mahakama inawatia hatiani,”anasema Hakimu Mkazi Bw. Obadia.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.