ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, December 12, 2012

ALLIANCE MWANZA YATWAA UBINGWA WA AFRIKA MASHARIKI ACADEMY

Alliance Academy ya jijini mwanza imeweza kujinyakulia vikombe viwili vya vijana chini ya miaka 12 na 14 pamoja na medali mbili za wafungaji bora kati ya michuano ya Afrika Mashariki ya Academy (nyumba ya vipaji) iliyokuwa ikitimua vumbi jijini Arusha. 

michuano hiyo iliyodumu kwa siku tatu tangu Disemba 7 na kukamilika Disemba 9 mwaka huu iliandaliwa na Academy ya features ya jijiji Arusha na kushirikisha nchi za Kenya, Uganda, Burundi, Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo ambao ni waalikwa pamoja na Tanzania ambao ni wenyeji.

Akizungumza mara baada ya kuwasili, katibu wa Alliance, Kessy mziray alisema ushindi wao ulitokana na kuzifunga timu za Burka mabao 3-0, Mambas ya uganda mabao 2-0, Olduvai ya Arusha mabao 3-0 na kufanikiwa kuingia fainali na Stars waliowakamua mabao 3-0 kwa vijana wenye umri chini ya miaka 14.

Mziray aliongeza kuwa kwa upande wa vijana wenye umri chini ya miaka 12 waliweza kuzifunga timu za Tacoda mabao 6-0, Olduvai ya Kenya mabao 2-0 na kufanikiwa kuingia fainali na Younglife  waliyoibanjua bao 1-0, hivyo kuibuka washindi wa michuano hiyo.


Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.