ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, March 15, 2012

MKUU WA MKOA WA MWANZA ERNEST NDIKILO ASHIRIKI MAADHIMISHO SIKU YA HAKI ZA MLAJI

Maadhimisho ya SIKU YA MLAJI DUNIANI ambayo 2012kitaifa yamefanyika jijini Mwanza katika viwanja vya Makongoro yamehitimishwa leo kwa maandamano yaliyofanyika kuanzia ofisi za Halmashauri ya jiji na kuishia eneo la tukio. Kauli mbiu ya mwaka huu ni FEDHA ZETU HAKI YETU (OUR MONEY OUR RIGHT).

Tuliongozwa na brass bendi ya vijana hawa.

Waandamanaji na ujumbe toka Baraza la ushindani.

Walaji wawakilishi toka shule za sekondari.

Mgeni rasmi Mkuu wa mkoa wa Mwanza Ernest Ndikiro pamoja na meza kuu walipokea maandamano hayo kwenye viwanja vya Makongoro.

"Natoa changamoto kwa NGO, msiishie kwenye kuunda asasi za kupambana na Ukimwi, Watoto yatima na mengine bali pia mjitokeze katika haya ili kuweza kushirikiana pamoja na serikali katika kumtetea mlaji kwani eneo hili linahitaji nguvu kubwa toka kwa asasi zisizokuwa za kiserikali kwani hatujamtetea mlaji vya kutosha" by mkuu wa mkoa.

Mh. Ndikilo akipata maelezo toka kwa bw. Joshua Msona Afisa mwandamizi mtetezi wa walaji pindi alipopata fursa ya kutembelea moja ya mabanda viwanjani hapo.

Wananchi wengi wamekuwa wakilanguliwa sana nauli kwa vituo mbalimbali vya daladala jijini hapa hivyo walipata fursa ya kupata chati za nauli kwa njia zote za safari toka katika banda la SUMATRA CCC kama mama huyu.

Wanazuoni nao wakizipitia chati za nauli.

"Aisee unaonaee.. jamaa wanatuibia" akiwa na wenzake alisikika akisema jamaa mwenye t-shirt ya njano mara baada ya kuipitia chati ya bei za nauli kwa ruti za ndani na nje ya jiji la Mwanza.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.