Maelfu ya wananchi wa Sudan Kusini wamekusanyika kushuhudia kupandishwa kwa bendera mpya ya nchi hiyo kuashiria kupata uhuru wake, katika mji mkuu Juba.Rais wa Sudan Omar al-Bashir na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ban Ki-moon ni miongoni mwa wageni waliohudhuria shughuli hiyo. Sudan Kusini limekuwa taifa jipya duniani usiku wa kuamkia Jumamosi, lengo ambalo limefikiwa kufuatia mkataba wa amani wa mwaka 2005 uliomaliza mapigano ya wenyewe kwa wenyewe yaliyodumu kwa miaka mingi.
Tupe maoni yako

0 comments:
Post a Comment