ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, December 9, 2025

MECHI ZA LEO UEFA NI PRESHA TUPU....


Italia kutakuwa na mechi ya kukata Inter Milan vs Liverpool ambao hivi karibuni wamekuwa na matokeo ambayo hayaridhishi kabisa kwani kwenye mechi 13 amabzo amecheza ameshinda 3 pekee. Mara nyingi hawa wawili kukutana ilikuwa kwenye fainali na Jogoo wa Anfield alipoteza. 

Vijana wa Diego Simeone, Atletico Madrid watakuwa ugenini kukiwasha dhidi ya PSV kutoka kule Uholanzi lakini pia imeweza kupata matokeo dhidi ya timu kubwa kwenye michuano hii. 

AS Monaco atakuwa nyumbani kupepetana dhidi ya Galatasaray ambao walipoteza mechi yao iliyopita wakiwa nyumbani. Mwenyeji yeye alitoa sare, hivyo pointi 3 ni muhimu kwa timu zote siku ya leo. 

Marseille yeye atakuwa kibaruani kumenyana vikali dhidi ya Union St.Gilloise ambao wanahitaji ushindi siku ya leo ili wasogee mbele kwenye michuano hii. Tofauti ya pointi kati yao hadi sasa ni hakuna kwani wote wana pointi sawa. 


Bayern Munich yeye atakipiga dhidi ya Sporting CP ambapo mpaka sasa kwenye mechi 8 ambazo amecheza amekusanya pointi 10 huku vijana wa Kompany wao wakichukua pointi 12. Mwenyeji ametoka kupoteza huku mgeni yeye akishinda. 

Kwa upande wa Chelsea wao watakuwa ugenini kukipiga dhidi ya Atalanta baada ya mechi iliyopita kushinda, halikadhalika kwa wenyeji nao walishinda. 


Vijana wa Hans Flick, FC Barcelona watakuwa nyumbani kusaka ushindi dhidi ya Eintracht Frankfurt ambao wana pointi 4 pekee hadi sasa huku Wacatalunya wao wakiwa na pointi 7. Barca wanahitaji ushindi kwa namna yoyote ile ili wajiweke kwenye nafasi nzuri ya michuano hii.  

Tottenham  Spurs atakuwa kibaruani kukipiga dhidi ya Slavia Prague ambao kwenye mechi 5 wameambulia pointi 3 pekee. Huku wenyeji wao wakiwa na pointi 8 hadi sasa. 

"MSIWE NA HOFU MWANZA HALI NI SHWARI CLIP INAYOSAMBAA NI YA TAREHE 31 OCTOBA 2025" RC MTANDA


NA ALBERT G. SENGO/MWANZA

🛑Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda, ametoa taarifa rasmi kuhusu hali ya usalama mkoani Mwanza, huku akikanusha vikali uvumi unaoenezwa mitandaoni kuhusu kuwepo kwa maandamano katika jiji hilo. Katika taarifa hiyo, Mhe. Mtanda ameeleza kwa uwazi kuwa video inayosambazwa mtandaoni si ya leo, bali ni tukio la zamani linalotumiwa kupotosha umma. 👉 Fuatilia video kamili kupitia #youtube chanel yetu hapa ujue alichokisema kwa kina Mkuu wa Mkoa juu ya usalama, uzushi wa maandamano, na msimamo wa serikali mkoani humo.
#mwanza #maandamano
Vituo vingi vya wauzaji wa mafuta na gesi jijini Mwanza, vimesitisha huduma kwa siku ya leo.
Hakuna huduma, hakuna pilikapilika kama ilivyozoeleka, vituo vingi vya wauzaji wa mafuta na gesi jijini Mwanza, vimesitisha huduma kwa siku ya leo.
Maduka mengi mtaa wa Nyerere yamefungwa.
Ni tofauti na ilivyozoeleka, leo magari ni ya kuhesabu katika barabara hii yenye pilika pilika hapa jijini Mwanza.
Muonekano wa barabara ya kuelekea Kirumba.
Muonekano wa barabara ya Makongoro uelekeo wa uwanja wa ndege jijini Mwanza.
Hakuna usafiri wa daladala zaidi ya pikipiki na bajaji, barabara ya Nyakato National kuelekea Igoma, Kisesa.
Watu wa kuhesabu barabarani.
Muonekano kutoka barabara ya Nyerere hii ni barabara ya kuelekea mitaa iliyozoeleka kwa pilikapilika nyingi ya Rufiji na Uhuru, lakini leo watu wachache na magari ya kuhesabu.
Hakuna huduma kwa siku ya leo.
Muonekano.
Muonekano.

Monday, December 8, 2025

VITALIS MAYANGA AFUNGIWA MECHI TANO NA KUTOZWA FAINI.

 

Mshambuliaji wa Mbeya City, Vitalis Mayanga amefungiwa kucheza mechi tano sambamba na kutozwa faini ya Tsh Milioni 1 kwa kosa la kumpiga kiwiko kwa makusudi beki wa kushoto wa Simba SC, Anthony Mligo.

Uamuzi huo umetolewa na Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu (TPLB) katika taarifa ya TPLB leo Desemba 8, 2025.

SIMBACHAWENE: HAKUNA TISHIO LA KUZIMWA INTERNET TANZANIA, HALI YA USALAMA NI SHWARI.

 

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene, amesema kuwa hatua ya kuzima mtandao wa intaneti nchini ni chaguo la mwisho kabisa, na kwa sasa hakuna sababu yoyote inayoashiria uwezekano wa TCRA kuchukua hatua hiyo kuelekea maadhimisho ya Uhuru kesho, Desemba 09, 2025.

Akizungumza leo, Desemba 08, 2025, Simbachawene amesema kuwa taarifa zinazosambaa mtandaoni kuhusu hofu ya kuzimwa kwa internet hazina msingi, kwani hali ya kiusalama nchini imo katika kiwango cha kuridhisha.

“Kuhusu kuzimwa mtandao, kwa sababu nyenzo kubwa inayotumika na hawa wanaharakati wa mitandaoni ni taarifa za taharuki… mpaka sasa hatujaona tishio lolote la kusema mtandao umekuwa tatizo,” amesema.

Ameeleza kuwa mitandao ya intaneti ina mchango mkubwa katika maisha ya kila siku ya Watanzania, kuanzia shughuli za kibenki, usafiri, mawasiliano hadi huduma mbalimbali za kijamii, hivyo serikali haina sababu ya kuuzuia bila msingi wa kiusalama ulio wazi.

“Tufahamu mtandao huu ndio unatumika kutoa huduma nyingi za kijamii. Kwa hiyo kuzima internet ni chaguo la mwisho sana pale ambapo hali ikiwa mbaya… lakini mpaka sasa, tunaoangalia usalama wa nchi, tunaona hali ni shwari,” amesema.

Simbachawene amesisitiza kuwa hadi sasa hakuna tishio lolote linaloweza kuilazimu TCRA kuzima huduma za intaneti, na Watanzania wanapaswa kuendelea na shughuli zao kama kawaida bila wasiwasi.

WANAFAMILIA 9 WALIOKUFA KATIKA AJALI WAKIENDA MAZISHI YA JAMAA YAO WAZIKWA PAMOJA

 

Waombolezaji wakitoa heshima za mwisho kwa ndugu na marafiki waliofariki kwa ajali hiyo. 


 Safu za majeneza meupe zilikaa kimya chini ya hema, picha ya kuhuzunisha ilinaswa na kusambazwa mtandaoni na mwandishi wa habari Bruce Kanzika. 

 Waombolezaji kutoka kila aina ya maisha walikusanyika kuwaaga waathiriwa ambao maisha yao yalikatizwa katika wakati mmoja, wa kuhuzunisha. 

 Msiba huo umetikisa kijiji cha Sango ambapo familia ilikuwa ikisubiri kwa hamu kuwasili kwa jamaa zao kwa mazishi ya bibi yao, Mama Perpetua Tsivona.

 Huenda swali likawa:- Jeh Waathiriwa walikuwa wakisafiri kwenda wapi?

Gari hilo, lililokuwa limebeba abiria 15, lilikuwa njiani kutoka Nairobi kwenda Lugari wakati ajali hiyo ilipotokea, na kuhitimisha safari iliyokusudiwa kuunganisha familia yenye huzuni. 

Simu iliyovunja mioyo ya familia nzima Kwa wazazi wa marehemu, maumivu bado hayajafikirika. Irene Haron, mama wa watoto tisa, alikumbuka kupokea simu kutoka kwa watoto wake, akimhakikishia kwamba walikuwa karibu na Naivasha na wangekuwa nyumbani alasiri. 

Muda mfupi baadaye, ulimwengu wake ulivunjika. “Sijui hata niseme nini. Watoto wangu wote tisa, wote wameenda,” alisema, akitetemeka huku akijitahidi kuelezea huzuni yake. “Kila ninapofikiria kuhusu hilo, mimi hutetemeka tu.” Mumewe, Mzee Haron Tsivona, anakumbuka kupokea simu kutoka kwa nambari ambayo hajui wakati yeye na jamaa wengine walikuwa wakiimba nyumbani kwa mama yake.

 Alipopokea simu, alikuwa polisi wa trafiki akimjulisha kwamba wanafamilia wake walikuwa wamehusika katika ajali. “Dakika chache tu mapema, watoto wangu walikuwa wamepiga simu kusema walikuwa karibu kurudi nyumbani,” alisimulia, sauti yake ikiwa nzito kwa kutoamini. 


Bajeti ya mazishi:-

 Wakati wanandoa hao wakikabiliwa na kazi isiyofikirika ya kuwazika watoto wao wote tisa, mzigo wa kifedha umeongeza safu nyingine ya uchungu. Familia ilikuwa na bajeti ya KSh milioni 4.5 kufidia gharama za mazishi, kiasi ambacho ni zaidi ya uwezo wao, na kulazimisha kutafuta msaada kutoka kwa wasamaria wema. 

Jamaa aliyetambuliwa kama Paulo Wawire alishiriki matumaini na ndoto ambazo watoto hao wa marehemu walikuwa nazo kwa wazazi wao, akiongeza kuwa walikuwa wameanza tu kupanga kujenga nyumba mpya kwa ajili ya wazazi wao. Miongoni mwa waliotembelea familia hiyo alikuwa Mbunge wa Lugari Nabii Nabwera ambaye alitoa mchango wa KSh milioni 1 kutoka kwa Rais William Ruto ili kusaidia mipango ya mazishi. 


Je, ajali hiyo ilikuwa na manusura? 

Huku Chevaywa akijiandaa kuwazika tisa wake, manusura wa ajali hiyo mbaya wanaendelea kulazwa hospitalini wakipokea matibabu. Kijiji hicho, kikiwa kimezidiwa na huzuni, kinashikilia umoja na maombi huku kikikabiliana na moja ya nyakati za giza zaidi katika historia yake. Kwa familia ya Haron, njia ya kuelekea uponyaji itakuwa ndefu, lakini jamii imeapa kuitembea nao, hatua moja, siku moja baada ya nyingine. 

IMBEJU NI ZAIDI YA MPANGO WA KUTOA MIKOPO CRDB BANK

 

  
Dar es Salaam – Katika hafla ya Marketers Night Out iliyofanyika jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation, Tully Esther Mwambapa, aliwasilisha mada iliyoangazia kwa kina mchango wa programu ya Imbeju katika kubadilisha maisha ya wananchi, hasa wanawake na vijana, kupitia uwezeshaji wa kiuchumi na kukuza ujumuishi wa kifedha nchini.

Akizungumza mbele ya wataalamu wa masoko, viongozi wa taasisi, wajasiriamali na wadau wa maendeleo, Mwambapa alisema Imbeju ni zaidi ya mpango wa kutoa mikopo pekee bali ni programu jumuishi inayolenga kujenga msingi imara wa ujasiriamali. Alieleza kuwa programu hiyo imejengwa juu ya nguzo tatu kuu; elimu ya ujasiriamali na uongozi, upatikanaji wa mitaji rafiki, pamoja na uunganishaji wa wajasiriamali na masoko pamoja na huduma rasmi za kifedha.
 
“Kupitia mafunzo ya vitendo, washiriki huwezeshwa kuendesha biashara zao kwa ufanisi zaidi, kutumia fursa za teknolojia, kufuatilia mapato na faida kwa weledi na kufanya maamuzi sahihi ya uwekezaji. mbinu hiyo imewezesha wajasiriamali wengi kuimarisha biashara zao na kuongeza ajira katika jamii”, alisema Mwambapa

Akizungumzia wanawake, Mwambapa alieleza kuwa wamekuwa walengwa muhimu wa programu kwani ndio mhimili wa ustawi wa familia na jamii. Wanawake wengi waliokuwa wakikabiliwa na changamoto za mtaji na elimu ya ujasiriamali sasa wameweza kuanzisha au kupanua biashara zao kupitia Imbeju, jambo lililosababisha kuongezeka kwa uzalishaji, kuboreshwa kwa kipato cha kaya na kuinuka kwa hali ya maisha ya familia zao. Alisisitiza kuwa uwekezaji kwa mwanamke mmoja hupelekea kuleta mafanikio kwa kizazi kizima.

Kwa upande wa vijana, alisema programu hiyo imekuwa chachu ya kubadilisha fikra bunifu kuwa miradi halisi katika maeneo ya teknolojia, kilimo-biashara, sanaa na biashara mtandao. Kupitia ushauri wa kitaalmu, mafunzo na ufadhili wa mawazo bunifu, vijana wengi wamepata uwezo wa kuzifikisha bidhaa zao katika masoko mengi zaidi kupitia majukwaa ya kidijitali, hivyo kuongeza ushindani na kupanua wigo wa biashara zao.
Mwambapa pia aligusia mchango wa Imbeju katika kukuza ujumuishi wa kifedha nchini kwa kuwawezesha wananchi waliokuwa nje ya mfumo rasmi wa benki kufungua akaunti, kujiwekea akiba, kukopa na kufanya miamala kwa urahisi zaidi baada ya kupata elimu ya kifedha. Kupitia ushirikiano wa CRDB Bank Foundation na Benki ya CRDB, huduma hizi sasa zimefika hata maeneo ya vijijini ambako upatikanaji wa huduma za kifedha ulikuwa mdogo awali.

Alisema hatua hiyo imeimarisha uthabiti wa biashara ndogondogo, kuongeza uwezo wa kujitegemea kwa wananchi na kuongeza mchango wa sekta hiyo katika ukuaji wa uchumi wa taifa.

Akihitimisha mada yake, Mwambapa alitoa wito kwa wadau wote kuendelea kuwekeza katika mipango inayowawezesha wanawake na vijana, akisisitiza kuwa mafanikio ya Imbeju ni ushahidi kuwa uwekezaji katika watu ndiyo msingi wa kujenga uchumi jumuishi, thabiti na wenye tija kwa kizazi cha sasa na kijacho.