ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, December 29, 2014

MSHINDI WA KWANZA WA SHINDANO LA TUTOKE NA SERENGETI AKIFURAHIA WIKIENDI MBUGANI

Mshindi wa kwanza wa shindano la “Tutoke na Serengeti” Bw.Hassan Mfaume akiwa na  rafiki yake kipenzi, Mohamedi Ally walipowasili katika hifadhi ya taifa ya Serengeti tayari kufurahia wikiendi yao kwa kutalii sehemu mbalimbali za hifadhi hiyo maarufu duniani. Safari hii inagharamiwa na Kampuni ya bia ya Serengeti.
Bw. Hassan na rafiki yake wakiwa ndani ya gari baada ya kuanza safari yao ya utalii ndani ya mbuga mashuhuri ya Serengeti mkoani Mara.
Hassan na rafiki yake wakipozi kwa ajili ya picha baada ya gari kujinasua kwenye matope..na hatimaye kuendelea na safari pembeni yao ni mwelekezi wao (Tour guide)
Hassan akitumia darubini kuangalia makundi ya wanyama pori ndani ya hifadhi hiyo.
Mshindi akiwa sehemu ya mandhari nzuri inayoitwa Ngorongoro plains ndani ya hifadhi ambapo waliweza kuangalia kundi kundi kubwa la simba na kupata maelezo zaidi kutoka kwa mwelekezi wao.
Mshindi akipata chakula cha jioni ndani ya Serengeti plains baada ya mzunguko wa siku nzima.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.