ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, January 17, 2011

MZEE MANDELA AVUMISHIWA KIFO...!

Habari zimetapakaa kutoka Johannesburg nchini Afrika kusini zikidokeza kuwa , uvumi umezagaa jijini humo kuwa Raisi wa zamani wa nchi hiyo Mzee Nelson Mandela yu taabani anaumwa na hali yake ni majaaliwa.Msemaji wa mfuko wa Nelson Mandela Sello Hatang amekanusha taarifa hizo siku ya jumamosi na kusema Mzee Mandela mwenye miaka 92 alikuwa katika mapumziko na mkewe Graca Machel na kwamba walikokwenda na wanachokifanya ni siri yao wawili na ni haki ya faragha kwa kila mwanadamu nayo inapaswa kuheshimiwa.

Hata hivyo kuna habari kuwa hali ya mzee huyo imezorota mno na wengine wamekuwa wakiwasiliana wakisema kuwa amekufa jambo ambalo limekanushwa vikali na watu wake wa karibu.

Hata hiyo vyanzo vya uhakika vilivyonukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari nchini humo vimeonyesha kuanza kukubaliana na uvumi huo.


Source wa habari: www.news24.com/SouthAfrica

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.