ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, April 20, 2018

CHANJO YA KUZUIA SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI SASA YATINGA MKOANI MWANZA


MKUU wa mkoa wa Mwanza John Mongella anatazamiwa kuwa mgeni rasmi wa uzinduzi wa Chanjo ya kuzuia saratani ya shingo ya kizazi, uzinduzi huo utakaofanyika mnamo tarehe 23 mwezi April 2018 katika Hospitali ya Wilaya ya Nyamagana unategemewa kuhusisha zaidi la wasichana 31,291 walio na umri kati ya miaka 9 hadi 14.

Katika semina kwa waandishi wa habari wa jijini Mwanza kwaajili ya kukuza uelewa wa ugonjwa huo wa saratani ya shingo ya kizazi mafunzo mafupi yametolewa ikiwa ni pamoja na taarifa ya uzinduzi.

Waandishi hao pia walipata fursa ya maswali na majibu.
Saratani ya shingo ya kizazi ni saratani ambayo hutokea kwenye shingo ya kizazi cha mwanamke - ambayo ni kiingilio kutoka uke hadi katika mfuko wa uzazi.
Ni moja kati ya zaidi ya aina 100 ya virusi vya human papilloma (HPV), ambavyo 13 vinasababisha saratani.
Pia aina fulani ya HPV vinaambukizwa kwa njia ya ngono.
Baadhi ya sababu za kupata ugonjwa huo ni kushiriki ngono ukiwa na umri mdogo, ukifanya ngono na washiriki wengi , kuvuta sigara na kuwa na virusi vya Ukimwi.
Dalili ni
  • kupata hedhi kwa mzunguko usio wa kawaida au kutoka damu baada ya kujamiana
  • maumivu ya mgongo, mguu na fupanyonga
  • uchovu, kupungua kwa uzito na kutokuwa na hamu ya kula
  • maumivu kwenye uke au kutoa harufu mbaya
  • kuvimba kwa mguu mmoja
Uchunguzi wa virusi hivyo unastahili kufanyika ili kuvigundua mapema. Chanjo za HPV ni hatua nyingine ya kuziuzi.
Matibabu kwa wagonjwa walio na virusi hivyo yanategemea na viwango vya virusi hivyo mwilini, hata hivyo yanaweza hitaji kutibiwa kwa njia ya upasuaji na kutoa sehemu au mfuko wa uzazi mzima au kutumia miyonzi.
Chanzo: Shirika la Afya duniani

Mambo kumi unayoweza kufanya kupunguza hatari ya kuugua saratani:

  • Usivute sigara wala kutumia tumbaku ya aina yoyote
  • Hakikisha nyumbani kwako hamna moshi
  • Kula chakula chenye afya
  • Kunyonyesha kunapunguza hatari kwa mama kuugua saratani
  • Hakikisha watoto wako wanapata chanjo dhidi ya hepatatis B na HPV
  • Epuka kuchomwa sana na miale ya jua, au tumia mafuta yanayo kukinga dhidi ya miale hiyo.
  • Punguza uchafuzi wa hewa ndani na nje ya nyumba
  • Jishughulishe kuupa mwili mazoezi
  • Punguza unywaji wa pombe
  • Jitahidi kufanyiwa ukaguzi wa mapema kutambua uwepo wa saratani.

BREAKING NEWS: MASOGANGE HATUNAYE


Msanii wa filamu za Kibongo na video queen maarufu, Agness Gerald Masogange amefariki dunia katika Hospitali ya Mama Ngoma Mwenge jijini Dar es Salaam kwa kile kilichoelezwa kwamba ni upungufu mkubwa wa damu. Masogange mzaliwa wa Mbeya, ameacha mtoto mmoja, Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi, Amina.

VIDEO: TAKUKURU YAWAFIKISHA MAHAKAMANI WALIOKUWA VIONGOZI CHAMA KIKUU CHA USHIRIKA NYANZA.


TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Mwanza, leo imewafikisha mahakamani waliokuwa viongozi waandamizi wa Chama Kikuu cha Shirika, Nyanza Cooperative Union (NCU), kwa tuhuma za ubadhirifu na ufujaji wa mali.

Kaimu Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Mwanza Susan Mwendi amesema, uchunguzi uliofanywa na TAKUKURU umeeleza kuwa aliyekuwa  Mwenyekiti Jacob Shibiliti na Makamu wake John Magulu ilibainika kati ya Januari 1, 2003 hadi Desemba 31, 2004  waliisababishia hasara NCU jumla ya Tshs.426,400,000 kwa kipindi hicho huku Makamu Mwenyekiti aliisababishia hasara shirika hilo takribani Tshs.332,640,000.

Mwendi amesema kuwa watuhumiwa waliisababishia NCU, hasara kinyume na Aya ya 10(1) ya jedwali la kwanza pamoja na kifungu cha 57(1) na 60(2) vya sheria ya Uhujumi uchumi, sura ya 200 kama ilivyofanyiwa marejeo mwaka 2002.

HATIMAYE WENGER AFUNGUA MLANGO WA KUTOKEA ARSENAL

KOCHA wa Arsenal, Arsene Wenger ameridhia kubwaga manyanga mwishoni mwa msimu huu baada ya majadiliano ya kina na uongozi wa klabu hiyo kongwe duniani.

“Baada ya kutafakari kwa kina kufuatia mazungumzo na klabu yangu, umefika wakati sasa nikae pembeni mwisho wa msimu huu, nina furaha sana kwa muda wote niliokaa hapa klabuni.

“Ninawashukuru wafanyakazi wenzangu, wachezaji, wakurugenzi na mashabiki kwa kuifanya klabu hii kuwa spesho, nimeitumikia kwa miaka mingi” amesema Wenger kwenye taarifa yake rasmi leo Ijumaa.

"I am grateful for having had the privilege to serve the club for so many memorable years.

"I managed the club with full commitment and integrity. I want to thank the staff, the players, the Directors and the fans who make this club so special.
"I urge our fans to stand behind the team to finish on a high. To all the Arsenal lovers take care of the values of the club.
"My love and support for ever."
Club owner Stan Kroenke said it was "one of the most difficult days we have ever had in all our years in sport".
In a statement, he said: "One of the main reasons we got involved with Arsenal was because of what Arsene has brought to the club on and off the pitch. His longevity and consistency over such a sustained period at the highest level of the game will never be matched.
"Arsene has unparalleled class and we will always be grateful to him. Everyone who loves Arsenal and everyone who loves football owes him a debt of gratitude.
"Three Premier League titles, including an entire season unbeaten, seven FA Cup triumphs and 20 successive years in the Champions League is an exceptional record. He has also transformed the identity of our club and of English football with his vision for how the game can be played."
Mr Kroenke said he had "high ambitions" to build on Wenger's "remarkable tenure" and wanted to "honour his vision" by making sure Arsenal could compete for the biggest trophies in the sport..

"We must now focus on making a strong finish to the season and ask our millions of fans around the world to join us in paying appropriate tribute to one of the greats of Arsenal's history and one of the greats of the game," he added.

RAIS MAGUFULI ASEMA HAKUNA UPOTEVU WA TRILIONI 1.5 KAMA INAVYODAIWA.


Rais John Magufuli amesema katika ripoti aliyopokea kutoka kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Prof. Mussa Assad haikuwa na upotevu wa fedha Tsh. Trilioni 1.5 kama inavyodaiwa.

Rais Magufuli amesema hayo leo wakati akiwaapisha majaji Ikulu Dar es Salaam na kueleza watu wanatumia uhuru wao vibaya na kupotosha kitu kilicholeta taharuki.

Rais Magufuli amesema mara baada ya kusikia kuna fedha zilizopotea alipiga simu kwa CAG kuhoji;.

“Mbona kwenye ripoti yako uliyonisomea hapa Ikulu hukunieleza juu wizi wa Trilioni 1.5 kwa sababu ungenisomea hapo siku hiyo hiyo ningefukuza watu , kama nimefukuza wakurugenzi watatu siku hiyo kwa kupata hati chafu hawa na Trilioni 1.5 uliwaficha wapi nimejaribu kusoma ripoti yako nimeperuzi kila kona sioni mahali zimeandikwa zimepotea trilioni 1.5 na Profesa Assad akaniambia hakuna kitu kama hicho na Katibu Mkuu akasema hakuna trilioni 1.5 iliyoibiwa na serikali” amesema Rais Magufuli

“Kwa sababu ya uhuru wa mtu kuandika chochote kwenye mitandao kwani hata ndege walisema mbovu hivyo ni kawaida ya uhuru huu, bahati nzuri Controller and Auditor General yupo hapa eti Controller and Auditor General kwenye ripoti yako tumeibiwa Trilioni 1.5? Sema hapa hapa watu wajue”

Baada ya kauli hiyo ya Rais Magufuli CAG alisema hakuna kitu kama hicho, pia katibu Mkuu alisema hakuna jambo kama hilo na kusisitiza kuwa Hazina wapo vizuri na wapo salama.

Thursday, April 19, 2018

LIVE - SHEREHE YA HARUSI YA ALIKIBA MOJA KWA MOJA KUTOKA MOMBASA KENYA


Historia imeandikwa leo kwa star wa muziki Tanzania, Alikiba kuchukua jiko kutoka mji wa Mombasa nchini Kenya. Ndoa tayari imefungwa leo Aprili 19, 2018 na kinachoendelea hivi sasa ni sherehe za ndoa hiyo. Tumeanza kwa kukuonesha jinsi mambo yalivyokuwa asubuhi wakati ndoa yenyewe ikifungishwa.

TAMKO LA CHAMA CHA MADEREVA WA SERIKALI TANZANIA LAIGONGA SERIKALI KATIKA HAYA



Ni katika mkutano wa chama cha madereva wa serikali mkoani Mwanza uliofanyika jana Aprili 15, 2018 katika ukumbi wa halmashauri ya Jiji la Mwanza ambao pamoja na mambo mengine ulilenga kujadili sakata la madereva wa vyeti feki pamoja na vyeti vya darasa la saba kuachishwa kazi. Said Yusuph Kapande ambaye ni Makamu Mwenyekiti Taifa wa Chama cha Madereva wa Serikali Tanzania anatoa tamko mbele ya waandishi wa habari jujunu Mwanza.

AIRTEL TANZANIA YAONGOZA KATIKA MITANDAO YA KIJAMII.

Mkurugenzi wa Masoko Airtel Tanzania, Bwn Isack Nchunda akiongea baada ya Airtel kuibuka kinara katika kutoa hudumia kupitia mitandao ya kijamii, akishuhudia Mkurugenzi wa Mawasiliano Airtel Tanzania, Bi Singano Mallya

Airtel Tanzania yaongoza katika mitandao ya kijamii
·        Yayapiku makampuni mengine yote ya simu Tanzania
Airtel Tanzania imetajwa kuwa moja ya makampuni bora ambayo yanajibu vizuri maswali ya mashabiki na wateja wake katika robo mwaka ya kwanza ya mwaka 2018.

Ripoti hii imetolewa na kampuni ya Socialbakers ambayo ni moja ya makampuni yanayoongoza duniani katika kutoa tathmini kuhusu namna makampuni mbalimbali yanawajibika katika kujibu maswali ya wateja wao katika mitandao ya kijamii. 

Kwa mujibu wa Socialbakers, tathmini ya robo hii ya mwaka ilifanyika kuanzia Januari 1, 2018 hadi Machi 31, 2018 na kuifanya Airtel Tanzania iibuke kidedea.

Kampuni hiyo ya Social bakers imekabidhi cheti kama ishara ya ushindi huu na kuonesha kuwa Airtel iliweza kujibu vizuri maswali ya mashabiki wake na wateja kupitia mtandao wa Face book kwa asilimia 98 na hivi kuyapiku makampuni mengine yote ya simu Tanzania. 

Mkurugenzi wa Masoko wa Airtel Tanzania, Bwn Isack Nchunda alisema wanajivunia kupata utambulizi huo na inaonesha jinsi gani wamekuwa wakijituma kuhakikisha wateja wao wanapata majibu ya maswali yao kwa wakati kupitia mitandao ya kijamii hususani Face book. 

“Tunayo faraja kuweza kutambuliwa kwa namna hii na sisi tunalo jukumu la kuendelea kuhakikisha wateja na mashabiki wetu wanapata majibu wanayohitaji kwa wakati na mitandao ya kijamii imeturahisishia kazi hii hususani kupitia Face book tumeweza kujibu maswali kwa haraka na kwa wateja wengi zaidi kwa wakati mmoja,” alisema. 

Mitandao ya kijamii kama Face book inatakiwa kutangazwa zaidi ili itumike kwa wingi kwani itapunguza usumbufu wa wateja kusubiri majibu kwa muda mrefu kama ilivyokuwa hapo awali ambapo walilazimika kupiga simu Airtel. “Kwa kupitia mitandao ya kijamii majibu yanatolewa hapo hapo na hili ndilo limetufanya tutambuliwe kwani tumeweza kutumia njia hii kwa ufanisi mkubwa na tathmini ya Socialbakers imeonesha kuwa katika robo ya kwanza ya mwaka huu tulijibu maswali kwa asilimia 98 na hivi kuibuka kidedea,” aliongeza Ndunda

Kwa mujibu wa Socialbakers, utambulizi huu unatokana na namna kampuni imeweza kujibu maswali ya watu kwa muda wa mwezi mitatu. Ili utambuliwe, lazima kampuniipokee maswali 50 kutoka kwa mashabiki katika robo husika na maswali hayo yaweze kujibiwa kwa zaidi ya asilimia 65. 

Socialbakers ni moja ya makampuni yanayoongoza duniani katika kutoa tathmini kuhusu namna makampuni mbalimbali yanawajibika katika kujibu maswali ya wateja wao katika mitandao ya kijamii hususani Face book, Twitter, Google+, LinkedIn na YouTube ili kusaidia makampuni kujua mafanikio ya kampeni mbalimbali kupitia mitandao hii.  

DIAMOND AKIRI TCRA! "MIMI NI BINGWA WA KIKI ILA......"


Diamond Akiri TCRA! "Mimi ni Bingwa wa Kiki Ila.." Saa chache baada ya wasanii wa muziki wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz na Nandy kuwasili katika ofisi za Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania 'TCRA' kwa ajili ya kuhojiwa kuhusiana na video zao za utupu, wasanii hao wameomba radhi kwa watanzania na serikali kwa ujumla. Wakizungumza na waandishi wa habari Diamond amesema wamejifunza mengi kutokana na makosa waliyotenda na kuahidi kuwa watakuwa mabalozi wazuri wa kuwaelimisha wasanii wengine juu ya matumizi ya mitandao kwa kuzingatia maadili.

HILI HAPA DUKA LA MITUPIO UWAPO JIJINI MWANZA.


















Uwapo jijini #Mwanza ondoa shaka na mitupio kwa #mitoko iwe #harusi au #dhifa za kitaifa au pozi za #Kula_batA yaani kodons kodons na skuna za kisasa ile #motO 
#AskwambieMtu ni @whitney_fashion_mwanza 
@whitney_fashion_mwanza 
Iwe mchana au Jioni kama hii fanya kupita au piga simu 0754511643

HISTORIA ISIYOFUTIKA WORLD CUP DHIDI YA SOKA LA DRC (ZAIRE)


 Uhuni haukuanza leo upo tangu enzi za wajomba, tena kipindi hicho kulikuwa na wababe kweli #UndavaUndava na uzinguaji #Gangwe Best time wasting tactic?
#SportsRipoti .
.
.
Timu ya Taifa ya Demokrasia ya Kongo (DRC) iliyokuwa Zaire zamani kwa mara ya kwanza ilijitokeza katika fainali za Kombe la Dunia mnamo mwaka  1974 ikiijulikana Zaire.

Vilevile ilikuwa ni timu wa kwanza kutoka ukanda wa Sahara barani Afrika kushiriki fainali za michuano ya Kombe la Dunia.
.

Pamoja na kusukuma kandanda safi na la kuvutia dhidi ya  Scotland na Brazil, timu hiyo katika michezo mitatu tu ya fainali hizo walikung'utwa jumla ya magoli 0-14. .

Way back Thursday #WBT aka #TBT

PIA CHEKI VIDEO YA CHINI ILIYOIGIZA TUKIO LA HASIRA KATIKA FREE KIK

NDOA YA ALIKIBA MJINI MOMBASA


NI FURAHA ILIYOJE! STAA wa Bongo Fleva, Ali Saleh Kiba ‘King Kiba’, amefunga ndoa na mchumba wake Amina Khalef, leo asubuhi, Aprili 19, mjini Mombasa nchini Kenya.

Hakika ni furaha, shangwe, nderemo na vifijo kwa maharusi, wanafamilia na mashabiki wa Kiba mara baada ya ndoa hiyo kufungwa katika msikiti wa Ummul Kulthum, mjini Mombasa.

Katika shughuli hiyo ya kihistoria kwa msanii huyo, Kiba ameandamana na mdogo wake, Abdul Kiba na na rafiki yake ambaye ni Gavana wa Mombasa, Hassan Joho ambaye ndiye amesimamia mipango yote ya harusi hiyo nchini humo.

Ilikuwa ni baada Koran kusomwa, na Sheikh Mohammed Kagera akakinyanyua kiganja cha Alikiba na kumuozesha kwa Amina Khalef.

“Mimi Ali Saleh nimekubali kumuoa Amina Khalef kwa mahari tuliyokubaliana na ikitokea sababu ya kuachana tuachane kwa wema,” amesema Kiba wakati akifunga ndoa yake.

Katika shughuli hiyo, Kiba alivaa joho na kilemba, alishika upanga kama desturi ya tamaduni ya zinavyomtaka na baada ya kutoka msikitini waalikwa wamekwenda nyumbani kwa ndugu wa Joho, Abu Joho, Kizingo.

RAIS MSTAAFU KIKWETE ATWAA TUZO MAREKANI.


Aliyekuwa rais wa awamu ya Nne wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Kikwete amekabidhiwa tuzo na chuo kikuu cha mjini New York, Marekani.

Dkt. Kikwete amekabidhiwa tuzo hiyo Africa House Presidential Award usiku wa Jumatano hii nchini humo.

Mhe. Kikwete amethibitisha hilo kupitia mtandao wake wa Twitter kwa kuweka picha hizo akikabidhiwa tuzo hiyo na kuandika, “The Africa House of the @nyuniversity awarded me with the Africa House Presidential Award this night.”

“I am grateful for this recognition. I dedicate it to all my fellow country men and women whose love and support for me has made me receive this award tonight,” ameongeza.

BIWI LA SIMANZI MWANAMKE AUAWA KIKATILI JIJINI MWANZA NA WATU WASIOJULIKANA


Mwanamke mmoja mkazi wa Kisoko Kata ya Luchelele wilayani Nyamagana mkoani Mwanza anayejulikana kwa jina la Anna Petro Titus (37) ameuawa kwa kukatwa mapanga na watu wasiojulikana.

Tukio hilo la kustusha limetokea ijumaa ya tarehe 13 majira ya saa 3usiku wakati mwanamke huyo akiwa na mwanaye nyumbani katika chumba chake kwenye himaya ya mama yake mzazi.

Kipi kilichotokea juu ya mauaji hayo FUATILIA SIMULIZI HII KWA VIDEO.


YANGA YATINGA HATUA YA MAKUNDI KOMBE LA SHIRIKISHO AFRIKA.


Klabu ya soka ya Yanga imefanikiwa kuingia hatua ya Makundi ya Kombe la Shirikisho barani Afrika baada ya kupata ushindi wa jumla wa mabao 2-1, licha ya kufungwa katika mchezo wa leo jioni na wapinzani wao Welayta Dicha.

Yanga imefungwa bao 1-0 kwenye mchezo uliomalizika jioni ya jumatano tarehe 17 April 2018 huko Ethiopia lakini imesonga mbele kutokana na ushindi wa mabao 2-0 iliopata nyumbani kwenye mchezo wa kwanza jijini Dar es salaam.

Hii sio mara ya kwanza kwa Yanga kutinga hatua ya makundi ambapo msimu wa 2015/16 iliingia katika hatua hiyo lakini ilimaliza katika nafasi ya mwisho na kushindwa kuendelea na michuano.

Yanga leo imecheza bila ya kocha wake mkuu George Lwandamina ambaye ameondoka klabuni hapo wiki iliyopita na kurejea kwenye timu yake ya zamani ya Zesco United ya Zambia.

RAIS MAGUFULI AFANYA UTEUZI WA WATU 10

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo April 18, 2018 ameteuwa watu kumi kushika nafasi mbalimbali akiwepo Prof. Idris Suleiman Kikula kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Madini.

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa uteuzi wa Prof. Kikula umeanza April 17, 2018


Wednesday, April 18, 2018

SHIRIKA LA KIMATAIFA LA WATER MISSION TANZANIA LAFANIKISHA MRADI WA MAJI SAFI NA SALAMA KIJIJI CHA KASANDA- KIGOMA

Kiongozi wa mbio za mwenge,Charles Kabeho akifungua bomba kuashiria uzinduzi wa mradi wa maji wa Kasanda iliofadhiliwa na Water Mission Tanzania.
 Shamrashamra za uzinduzi wa mradi
Kiongozi wa mbio za mwenge, Charles Kabeho, akiongea na wananchi wakati wa uzinduzi wa mradi wa maji Kasanda,(kushoto) ni Mkurugenzi wa Kanda wa shirika la kimataifa la Water Mission, Will Furlong

Shirika la kimataifa la Water Mission Tanzania lafanikisha mradi wa maji safi na salama katika Kijiji cha Kasanda

Wakazi wa kata ya Kasanda, wilayani Kakonko mkoani Kigoma, jana,wameanza kupata maji safi na salama kutokana na kuzinduliwa kwa mradi mpya wa maji chini ya ufadhili wa Shirika la kimataifa la Water Mission Tanzania. Mradi huu utanufaisha zaidi ya kaya 729 zinazoishi maeneo hayo.

Miradi ya Kakonko na Kasanda, ni miongoni mwa miradi zaidi ya 20 ya kuwapatia wananchi maji safi na salama ambayo imetekelezwa na shirika la Water Mission Tanzania tangu mwaka 2014. Miradi ya Kasanda na Kakonko ni tofauti na ile iliyotekelezwa maeneo mengine kwa kuwa iko katika maeneo yaliyopo karibu na kambi ya wakimbizi ya Mtendeli.

Mkurugenzi wa Kanda wa shirika la kimataifa la Water Mission, Will Furlong alisema “Water Mission Tanzania, kupitia ufadhili wa taasisi ya Poul Due Jensen Foundation ambayo zaidi inajulikana kama, Grundfos Foundation, imewezesha ufanikishaji miradi 8 ya maji safi na salama kwa jamii mbalimbali nchini. Mradi mwingine wa Zeze mkoani Kigoma nao tayari umezinduliwa mwezi huu. Mashirika ya Water Mission Tanzania na Grundfos Foundation, yanashirikiana kuhakikisha huduma za maji safi na salama zinafikia jamii zenye changamoto katika kanda ya Afrika Mashariki”.

Akiongea wakati wa uzinduzi wa mradi huu mkubwa wa maji ulioambatana na sherehe za mbio za Mwenge katika kata hiyo,Kiongozi wa mbio za mwenge,Charles Kabeho,alisema kuwa kuzinduliwa kwa mradi huo ni jambo la kihistoria kwa wakazi wa eneo hilo ambalo kwa muda mrefu wamekuwa wakikabiliwa na changamoto ya kupata maji safi na salama.

“Kwa niaba ya serikali napenda kutoa shukrani kwa wadau wa maendeleo wanaounga mkono jitihada za serikali katika kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazokabili jamii kama ambavyo hawa wenzetu wa Water Mission Tanzania ,wamekuwa mstari wa mbele kufanikisha miradi ya maji sehemu mbalimbali hapa nchini”alisema Kabeho.

Alisema kero ya ukosefu wa maji safi na salama kwa muda mrefu ilisababisha akina mama kutembea mwendo mrefu kutafuta maji sambamba na wananchi wengi kuathirika kwa kupata magonjwa mbalimbali kutokana na kutumia maji yasio salama kwa matumizi ya binadamu.

Kabeho,alitoa wito kwa wakazi wote wa eneo hilo kujiona ni sehemu ya mradi huu na kuhakikisha wanatunza miundo mbinu ya mradi wakati wote sambamba na kutoa ushirikiano kwa wataalamu wanaofanya ushauri wa uendeshaji mradi.

TAMASHA LA AMKA KIJANA, TUIJENGE IRINGA YETU...

Mkuu wa wilaya ya Iringa Mhe. Richard Kasesela akimtambulisha mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Amina Masenza (mwenye ushungu) huku mwenyekiti wa Uzalendo Kwanza, Steve Nyerere akifuatilia kwa karibu wakati wa Tamasha la Amka Kijana, Tuijenge Iringa Yetu lililofanyika uwanja wa MwembeTogwa, Iringa mwishoni mwa wiki iliyopita.
Mkuu wa wilaya ya Iringa Mhe. Richard Kasesela (kushoto) akifurahia burudani iliyokuwa ikitolewa na msanii wa Muziki wa Singeli, Dulla Makabila wakati wa Tamasha la Amka Kijana, Tuijenge Iringa Yetu lililofanyika uwanja wa MwembeTogwa, Iringa mwishoni mwa wiki iliyopita.
 Msanii wa Bongo Fleva, Nuh Mziwanda nae hakuwa nyuma kutoa burudani. Mkuu wa wilaya ya Iringa Mhe. Richard Kasesela akizungumza na wana-Iringa waliojitokeza katika amasha la Amka Kijana, Tuijenge Iringa Yetu lililofanyika uwanja wa MwembeTogwa, Iringa mwishoni mwa wiki iliyopita. Mwenyekiti wa Uzalendo Kwanza, Msanii wa Bongo Movies, Steve Nyerere ambao ndiyo waandaaji wa Tamasha la Amka Kijana, Tuijenge Iringa Yetu akizungumza machache na wakazi wa Iringa juu ya kutunza Amani, Upendo na Mshikamano wetu katika uwanja wa MwembeTogwa, Iringa mwishoni mwa wiki iliyopita.

Mkuu wa wilaya ya Iringa Mhe. Richard Kasesela akiwatambulisha wasanii wa Bongo Movie waliofika katika Tamasha la Amka Kijana, Tuijenge Iringa Yetu lililofanyika uwanja wa MwembeTogwa, Iringa mwishoni mwa wiki iliyopita. Mratibu wa Tamasha la Amka Kijana, Tuijenge Iringa Yetu, Msanii wa Bongo movies, Single Mtambalike (Rich Rich) akizungumza machache wakati wa tamasha hilo lililofanyika uwanja wa MwembeTogwa, Iringa mwishoni mwa wiki iliyopita. Msanii maarufu wa Bongo Movies Jacob Steven 'JB ' akieleza machache. Msanii maarufu wa Bongo Movies Jacob Steven 'JB ' akimtambulisha msanii mwenzake Weru Sengo. Msanii wa Kundi la Ze Komed akitoa burudani. Mchekeshaji maarufu, Mama Asha Boko akitoa burudani. Dj Choka nae alipata wasaa wa kutoa neno kwa wana-Iringa. Msanii wa Bongo Movies, Anti Ezekiel akiwasalimu wakazi wa Iringa.
Msanii wa Bongo Movies, Jackline Wolper toa burudani.
Wanamuziki wa bendi ya Fm Academia Wazee wa Ngwasuma wakitoa burudani.
Wasanii wa Bongo movies wakipata picha ya pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Mhe. Richard Kasesela na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Amina Masenza na viongozi wengine wa Mkoa mara baada ya kumalizika kwa Tamasha la Amka Kijana, Tuijenge Iringa Yetu.