ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, March 10, 2018

MSHINDI WA DROO YA KAPENI YA MALENGO NBC APATIKANA TARIME


NA ZEPHANIA MANDIA WA G.SENGO TV

Taasisi za kifedha zimekuwa zikitoa elimu kwa wananchi kuhusu uwekaji akiba, matumizi bora ya fedha na kuhimiza kutumia benki kwaajili ya usalama wa fedha zao.
Benki ya NBC ambayo ni mojawapo ya taasisi ambazo zimekuwa zikihamasisha wananchi kujiwekea akiba kupitia Malengo akaunti imechezesha draw maalum kwa washiriki wa kampeni hiyo iliyofanyika kwa kipindi cha miezi mitatu katika kanda ya ziwa. 
Katika kampeni ya akaunti ya malengo iliyoendeshwa na benki hiyo kwa nchi nzima,kwa upande wa kanda ya ziwa mkazi wa Tarime, TUNDA MACHAGE ameibuka mshindi kwa kujinyakulia gari dogo maarufu kama “kirikuu”  

Meneja wa kampeni ya wekeza NBC MTENYA CHEYA,Nae akasema kuhusu droo hiyo (CHEKI video).






TUIMARISHE USAWA WA KIJINSIA NA KUWEZESHA WANAWAKE VIJIJINI-DC MCHEMBE

Mkuu wa Wilaya ya Gairo, Mhe. Siriel Mchembe akimtambulisha kwa wananchi Mkuu wa dawati la Jinsia Polisi Gairo, Mrakibu Msaidizi wa Jeshi la Polisi, Hope Kimaro wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani iliyofanyika Wilayani humo.
Mgeni rasmi Mhe. Mchembe akipokea taarifa ya Wanawake Gairo kutoka kwa Mkurugenzi wa Halmashauri Gairo, Agnes Mkandya.
Uongozi wote wa Wilaya ya Gairo, upande wa Chama na Serikali ukielekea kwenye kupanda miti kuashiria alama ya uhai mpya kwa wanawake waliokata tamaa.
Viongozi wakiwa fuatilia.
Mkurugenzi wa Halmashauri Wilaya ya Gairo, Agnes Mkandya akitoa salamu.
Mkurugenzi wa Halmashauri, Mhe. Rahel Nyangasi akitoa salamu.
Viongozi Wanawake wa Wilaya ya Gairo wakiongozwa na mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Gairo, Mhe. Siriel Mchembe (wa pili toka kushoto),  Mwenyekiti wa Halmashauri  Mhe.  Nyangasi (watatu kushoto) na Agnes Mkandya  wakiimba wimbo maalumu kwa ajili ya siku ya Wanawake Duniani. Wilaya ya Gairo inaendeshwa na wanawake kwa asilimia zaidi ya 95 (tisini na tano).
Wanawake wakipima VVU wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani iliyofanyika Wilayani humo.
Akinababa nao walijitokeza kuomba msaada wa kisheria.

Na Mwandishi Wetu.

Wilaya ya Gairo imefanya maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani Machi 8 kupanda miti ili kuashiria uhai kwa wanawake waliokata tamaa.

Zoezi hilo liliongozwa na mgeni rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Gairo, Mhe. Siriel Mchembe na wanasheria wanawake sita akiwemo Mwanasheria wa Manispaa Mvomerowaliweza kusikiliza kero za muda mrefu za wanawake.

Masuala  yaliyoangaliwa katika maadhimisho hayo ni  migogoro ya ardhi, mirathi, unyanyasaji kijinsia,  ukeketaji na kesi za mimba za utotoni ambapo zaidi Wanawake zaidi ya 65 waliweza kuhudumiwa.

Kauli mbiu katika maadhimisho hayo wakati wakiendelea katika Uchumi wa Viwanda, "Tuimarishe usawa wa kijinsia na kuwezesha wanawake vijijini", ambapo ulipokelewa kwa shangwe na wanawake kijiji cha Kisitwi jambo lililomvutia Mkurugenzi Bi. Agnes Mkandya na kugawa miche ya korosho zaidi ya  elfu 40, mbegu za pamba na kahawa. 

Mhe. Mchembe alisisitiza wanawake kulima Kilimo cha Kibiashara ili kuinua kipato na uchumi wao waondokane na utegemezi.

Mkuu wa Wilaya huyo ameziomba  Taasisi za kifedha NMB na CRDB kutoa mikopo kwa wanawake yenye riba nafuu, aidha kabla ya mkopo wanawake wapewe Elimu ya fedha,   masoko,   vifungashio, Sheria mbambali na ujasiriamali katika mapana yake.

RAIS MAGUFULI AZINDUA JENGO JIPYA LA TAWI LA CRDB WILAYANI CHATO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi mbalimbalia Chato waliohudhuria kwenye uzinduzi wa jengo jipya la Benki ya CRDB tawi la Chato, Leo Machi 2018
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli akikata utepe ishara ya uzinduzi wa jengo jipya la Benki ya CRDB tawi la Chato, Leo Machi 2018
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi mbalimbalia Chato waliohudhuria kwenye uzinduzi wa jengo jipya la Benki ya CRDB tawi la Chato, Leo Machi 2018

Na Mathias Canal, Chato-Geita

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Maguguli Leo 9 Machi 2018 amezindua jengo jipya la Benki ya CRDB Tawi la Chato Mkoani Geita.

Akizungumza katika uzinduzi huo Mhe Dkt. Magufuli amesema kuwa uwepo wa Benki hiyo utarahisisha huduma za uhifadhi fedha kwa wafanyabiashara wa samaki Wilayani Chato sambamba na wananchi ambao kwa kiasi kikubwa katika msimu wa Kilimo wamenilima Pamba kwa wingi.

Ameipongeza Benki Kuu ya Tanzania (BOT) kwa kuzifungia baadhi ya Benki nchini na kuzipa onyo zingine ambazo zilikuwa zinafanya kazi kwa mazoea na kwenda kinyume na utaratibu wa sheria za uendeshaji.

Alisema ni bora kuwa na Benki chache nchini ambazo zinaweza kuwahudumia wananchi wengi hususani masikini kama ilivyo CRDB ambayo imewafikia kwa kiasi kikubwa wananchi vijijini hivyo kuendelea kuzifungia Benki zote ambazo zimeshindwa kuendesha vyema shughuli zake na kusalia kufanya huduma Jijini Dar es salaam pekee.

Rais Magufuli ameiomba benki ya CRDB kupunguza riba ya mikopo kwani ni asilimia 16 pekee ya watanzania ndio wanaohudumiwa kwenye Benki nchini hivyo ili wananchi wote waweze kukopa na kuweka mitaji yao midogo kwa ajili ya faida yao ya Sasa na badae ni lazima kuwa na riba rafiki kwa wananchi.

JPM ameipongeza Benki hiyo kwa kuajiri wafanyakazi wapatao 3200 tangu ilipoanza rasmi nchini mwaka 1972 wakati wa utawala wa serikali ya awamu ya kwanza chini ya hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere aliyeielewa dhana halisi ya kuwasaidia wananchi vijijini kutokana na usumbufu mkubwa wanaoupata katika huduma za kifedha.

Alisema kuwa anayo imani kubwa na Benki ya CRDB kwani naye ni mteja wa benki hiyo hivyo ili kuendeleza mahusiano mema tayari seikali imelipa Deni lote la shilingi Bilioni 16 ambalo ilikuwa inadaiwa na benki hiyo kutokana na mikopo katika miaka ya nyuma.

Katika hatua nyingine Rais Magufuli amewahamasisha wananchi kutunza fedha zao benki na kuachana na dhana ya kuhifadhi fedha majumbani jambo ambalo ni hatari kwa usalama wa fedha hizo na maisha yao wenyewe.

Mhe Magufuli amesisitiza watanzania kuwa wazalendo huku akisema kuwa anatambua kuwa wapo baadhi ya wananchi ambao wamesalia na jukumu la kuandika katika mitandao na vyombo vya habari mambo ambayo ni kinyume na utendaji wa serikali jambo ambalo ni uchonganishi dhidi ya wananchi na serikali yao.

Aidha, Mhe Rais Magufuli alikataa ombi la Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Tanzania Dkt Charles Kimei aliyetaka Benki hiyo kuitwa CRDB JOHN POMBE MAGUFULI-CHATO huku akisema kuwa isalie kuitwa CRDB tawi ka CHATO.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Tanzania, Dkt Charles Kimei ametoa pongezi kwa Rais Magufuli kwa kukubali kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa Benki hiyo huku akielezea namna ambavyo amekuwa na dhamira ya dhati ya kuwainua watanzania kupitia rasilimali zao jambo ambalo litawanufaisha na kuwainua kiuchumi.

Alisema kuwa Benki hiyo itaendelea kubuni njia nzuri za mikopo huku akisisitiza kuwa Benki hiyo kuendelea kuwasaidia wananchi kupitia SACCOS zao kupata mikopo nafuu ili kujinufaisha kwa kuwa na uchumi imara utakaowawezesha kukuza biashara zao.

Sambamba na hayo pia amekubali ombi la Mbunge wa Jimbo la Chato Mhe Medard Kalemani ambaye ni Waziri wa Nishati la kujenga uwanja wa kisasa wa Mpira wa miguu ambapo kwa niaba ya Benki hiyo Mwenyekiti wa Bodi ya wadhamini Benki ya CRDB Tanzania Ndg Martin Mmari amekabidhi Hundi la Shilingi Milioni 50 kwa ajili ya hatua za mwanzo za kuanza ujenzi wa uwanja huo huku akiahidi Benki hiyo kuwa wadhamini wa timu ya mpira wa miguu ya wilaya ya Chato.

Dhifa ya uzinduzi wa Benki hiyo ulihudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Waziri Wa Nishati Mhe Medard M.Kalemani (Mb), Naibu Waziri wa Madini Mhe Doto Mashaka Biteko (Mb), Mkuu Wa Mkoa Wa Geita Mhandisi Robert Gabriel, Naibu Waziri Wa fedha na Mipango Dkt Ashatu Kijazi (Mb), Naibu Gavana Wa Benki Kuu Tanzania Dkt Bernard Yohana Kibese, Balozi Wa Denmark nchini Tanzania Mhe Einar Hebogard Jensen, Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi CRDB Tanzania Ndg Martin Mmari, Mkurugenzi Mtendaji CRDB Tanzania Dkt Charles Kimei, na Wabunge wa majimbo mbalimbali ikiwemo jimbo la Busanda na Mbogwe.

Friday, March 9, 2018

VIDEO FULL:- SHINYANGA YAONGOZA KWA MIMBA ZA UTOTONI.


Zaidi ya wanafunzi elfu 66 wa shule za msingi na sekondari nchini wamekatisha masomo yao baada ya kubemba mimba huku kati yao wanafunzi elfu saba wakitoka mkoani Mwanza ambao ni asilimia 37 huku mkoa wa Shinyanga ukiongoza kwa kuwa na asilimia 59 ikifuatiwa na Tabora yenye asilimia 58 Mara asimilia 55 na Dododma asilimia 51 ukiwa ni utafiti wa taasisi zisizo za kiserikali zinazo jishughulisha na kubaini na vitendo vya ukatili. 

YANGA YAICHARAZA KAGERA 3-0


Yanga imerejea katika nafasi ya pili jioni hii baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Kagera Sugar FC, mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Mechi hiyo iliyopigwa Uwanja wa Taifa Dar es Salaam, ilimalizika dakika 45 za kwanza kukiwa hakuna timu iliyoweza kuona lango la mwenzake.

Kipindi cha pili kilikuwa na neema kwa Yanga, ambapo mnamo dakika ya 53, Ibrahim alifunga bao la kwanza kwa njia ya penati, baada ya beki wa Kagera kuunawa mpira eneo la hatari.

Yanga walizidi kuamka zaidi haswa kuelekea dakika za mwisho kipindi cha pili, ambapo katika dakika ya 77, Yusuph Mhilu, alifunga bao la pili na kufanya ubao wa matokeo usomeke kwa mabao 2-0.

Kazi nzuri ya Mhilu ilizidi kuzaa matunda tena, ambapo mnamo dakika ya 88, Juma Shemvuni alijifunga, kufuatia kazi nzuri ya Yusuph Mhilu, baada ya kupiga shuti kali ambalo lilisababisha Shemvuni kujifunga.

Mpaka Mwamuzi anapuliza filimbi ya mwisho, Yanga walikuwa mbele kwa mabao 3-0 dhidi ya Kagera Sugar.

Matokeo hayo sasa yameirejesha Yanga mpaka nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu Bara, na kuifanya ibakize alama 3 pekee kuifikia Simba inayoongoza ligi.

Yanga sasa ina pointi 43 ikiwa nafasi ya pili, huku Simba ina alama 46, na Azam imeshuka hadi nafasi ya tatu ikiwa na alama zake 42.

WAKURUGENZI WA HALMASHAURI MKOANI GEITA WAKUMBUSHWA KUTENGA FEDHA KWA AJILI YA WABAWAKE


Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe Robert Gabriel akisisitiza umuhimu wa kuheshimu wanawake wakati akihutubia wananchi waliojitokeza kwenye maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani yanayoadhimishwa kimkoa katika Wilaya ya Bukombe Mkoani humo, Jana 8 Machi 2018. Picha Zote Na Mathias Canal-Wazo Huru Blog
Baadhi ya wanawake Wilayani Bukombe wakifatilia maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani yanayoadhimishwa kimkoa katika Wilaya hiyo Mkoani humo, Jana 8 Machi 2018.
Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe Robert Gabriel akiongoza zoezi la ukataji keki kabla ya kuhutubia wananchi waliojitokeza kwenye maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani yanayoadhimishwa kimkoa katika Wilaya ya Bukombe Mkoni humo, Jana 8 Machi 2018.
Mbnge wa Jimbo la Bukombe ambaye pia ni Naibu Waziri wa madini Mhe Doto Mashaka Biteko akichangia shilingi 500,000 kuunga mkono harambee iliyoendeshwa na Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe Robert Gabriel ambaye naye alichangia shilingi laki tano kwa ajili ya jukwaa la wanawake Jimbo la Bukombe, Jana 8 Machi 2018

Na Mathias Canal, Geita

Wakurugenzi wa Halamshauri za Wilaya katika Mkoa wa Geita wamekumbushwa kutekeleza wajibu wao kwa kutenga fedha asilimia 4 kwa ajili ya mfuko wa maendeleo ya wanawake, asilimia 4 kwa ajili ya mfuko wa maendeleo ya vijana na asilimia 2 kwa ajili ya watu kwenye ulemavu.

Wakurugenzi hao wametakiwa kuongeza kasi katika kuendelea kuchambua na kutambua vikundi vya wanawake na vijana vyenye mwelekeo wa kuzalisha Mali ghafi kwa ajili ya kulisha viwanda vidogo na vya kati ili kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe Robert Gabriel wakati akihutubia wananchi waliojitokeza kwenye maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani yanayoadhimishwa kimkoa katika Wilaya ya Bukombe.

Alisisitiza kuwa vikundi hivyo vinapaswa kujengewa uwezo wa kifedha, mafunzo pamoja na vifaa na hatimaye viweze kuchangia katika azma ya Serikali ya Tanzania ya uchumi wa viwanda kwani kupitia fursa hizo wanawake wengi watajiajiri na kuajiri watu wengine katika sekta isiyo rasmi.

Alisema kuwa sambamba na kuwajengea uwezo wanawake lipo jukumu la kuwalinda wanawake hao pamoja na wasichana dhidi ya vitendo vya ukatili kimwili kama vipigo, ubakwaji, ndoa za utotoni na kuwarubuni kimapanzi wabinti wadogo.

Aidha, amezitaka mamlaka zote ndani ya Mkoa wa Geita kuhakikisha zinatoa ushirikiano kwa wajumbe wa kamati zinazoundwa katika ngazi zote ili kwa pamoja kuhakikisha vitendo vyote vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto vinatokomezwa.

Katika hatua nyingine Mhe Gabriel amezitaka Halmashauri za Wilaya kushirikiana na wadau mbalimbali kutenga bajeti na kuendelea kuweka mipango shirikishi ya kusaidia kutatua changamoto zinazowakabili wanawake na wasichana ikiwa ni pamoja na kuendelea kutoa elimu kwa jamii kuhusu umuhimu na usalama wa mtoto wa kike na kulinda mustakabali wake kwa kumuwezesha kiuchumi, kielimu, kiafya na kumlinda dhidi ya vitendo vya ukatili kimwili.

Alisema kuwa kauli mbiu ya Kitaifa kwa mwaka huu ni "KUELEKEA UCHUMI WA VIWANDA: TUIMARISHE USAWA WA KIJINSIA NA UWEZESHAJI WANAWAKE VIJIJINI" imeakisi dira ya Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe. Dkt John Pombe Magufuli kwa muktadha wa kuhakikisha Tanzania inakuwa ni nchi ya uchumi wa viwanda.

Alisema Serikali inatambua nguvu na ufanisi wa wanawake kwani kupitia vikundi vya kiuchumi, VICOBA, SACCOS na vikundi vya kijamii wamekuwa wakijihusisha na shughuli mbalimbali za kiuchumi; Uchakataji wa malighafi ili kuongeza thamani, biashara ndogondogo, ufugaji ushonaji nguo, kilimo cha mazao, bustani za mbogamboga na matunda na nyinginezo.

Katika maadhimisho hayo Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe Doto Mashaka Biteko amewapongeza wanawake Duniani kote kwa maadhimisho hayo ya siku muhimu kwao huku akiahidi kuongeza ushirikiano kupitia vikundi vya mbalimbali ambavyo ni msingi wa ustawi na uimara wa Jumbo hilo na Taifa kwa ujumla wake.

Sambamba na hayo pia Mhe Biteko amechangia shilingi laki tano (500,000) kwa kuunga mkono harambee iliyoendeshwa na Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe Robert Gabriel ambaye naye alichangia shilingi laki tano kwa ajili ya jukwaa la wanawake Jimbo la Bukombe.

Thursday, March 8, 2018

KOROMIJE WAFUNGUKA SABABU SUGU NA VIKWAZO KWA MAENDELEO YA WANAWAKE VIJIJINI KUELEKEA UCHUMI WA VIWANDA.


SIKU ya kimataifa ya wanawake imeadhimishwa leo Alhamisi, duniani kote kwa kufanyika shughuli mbalimbali katika nchi tofauti huku kukitolewa mwito kwenda kwa makundi yote kuhusu nafasi ya mwanamke katika jamii mbalimbali.

Wanawake wa mkoa wa Mwanza nchini Tanzania wameiadhimisha siku hiyo katika kijiji cha Koromije kilichopo wilayani Misungwi mkoani Mwanza, maadhimisho yaliyofanyika kwenye viwanja vya shule ya Sekondari Koromije kwa kuzungumzia changamoto zinazo wakabili wanawake wa Kitanzania hasa wa vijijini katika kujikwamua kiuchumi, hasa ikizingatiwa kuwa kauli mbiu ya mwaka huu nchini hapa ilijikita kumuangazia zaidi mwanamke wa kijijini.

Kauli mbiu ya mwaka huu inasema 'Kuelekea Uchumi wa Viwanda, Tuimarishe Usawa wa Kijinsia na Uwezeshaji Wanawake Vijijini'.

Hakika Imekuwa siku ya utofauti na faraja kubwa kwani Shirika la Kutetea Haki za Wasichana na Wanawake KIVULINI, chini ya Mkurugenzi wake Yassin Ally imeratibu vyema Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, ngazi ya mkoa wa Mwanza.

Mgeni rasmi alikuwa Mkurugenzi Msaidizi wa Jinsia wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Constansia Gabusa. 

Kwenye kusanyiko hilo wanawake wameketi kwa makundi, wakitabasamu na nyuso za furaha lakini vichwani mwao kukiwa na mawazo yaliyogubikwa na manung'uniko kutokana na changamoto nyingi zinazo zorotesha ushiriki wao kuelekea Tanzania ya viwanda.

Moja ya Changamoto kubwa ambazo zimeainishwa ni namna ya kupata mitaji kwa ajili ya kuendesha maisha yao kwa wanaotaka kujikita kwenye ujasiriamali husasani upatikanaji wa mikopo yenye riba nafuu.

Teresia Mnaku ni mwanamama mjasiliamali kutoka wilayani Misungwi ambaye alipewa dhamana na wawakilishi wa vikundi vingine kusoma Risala ya maadhimisho, naye anasema "Unakuta Taasisi fulani inatoa mikopo lakini ile riba inakuwa ni kubwa, mama anatakiwa kurejesha  kiasi kikubwa ambacho kwa uwezo wake kwa kipindi kilichowekwa inamuwia vigumu kutimiza, hatma yake muda wa kurejesha mkopo ukiisha, wanakamata mali zake pamoja na uwekezaji wake naye anarudi katika umasikini zaidi kuliko ule aliokuwa nao" 

"Mikopo mingi hutolewa na Ofisi za Halmashauri, ule umbali kutoka kijijini hadi ofisi za mikopo una athari kubwa kwani wadau wa vikundi wasio na mitaji hulazimika kusafiri kwa gharama kubwa kutoka eneo moja hadi jingine, mpaka mkopo utoka wanajikuta tayari wamesha tumia nusu ya fedha ya mkopo huo waliokuwa wakiufuatilia. Ili kuleta maana, nashauri hawa wadau wa mikopo wasogeze huduma hizo vijijini" aliongeza Bi. Teresia.

Nayo maeneo ya kufanyia bishara yanetajwa kama kizuizi kwa wanawake kufanikiwa kuyafikia malengo kwani maeneo mengi ya biashara vijijini siyo rasmi, yana vizuizi vingi na migogoro baina ya watendaji wake na wasimamizi wa sheria, wakati wowote maamuzi yanafanyika kusitishwa matumizi au marufuku kutumika kwa kufanyia biashara.

Hii ina athari kubwa hasa kwa waakinamama ambao wengi wao wanabidhaa zinazo hitaji nguvu ya ziada kuhamishika kama vile mama lishe ambao wengine huishia kumwagwa bidhaa zao na kupoteza mitaji.

Upatikanaji wa leseni na gharama zake hazilingani hata kiduchu na biashara zao kuanzia mitaji hadi vipato.