ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, August 1, 2018

MABULA KUPELEKA BUNGENI AJENDA YA WAFANYABIASHARA WA FILAMU



ZEPHANIA MANDIA/GSENGOtV

Mbunge wa jimbo la nyamagana mkoani Mwanza, stanslaus Mabula, amesema anakusudia kupeleka ajenda ya wafanyabiashara wa filamu nchini kusaidiwa kutengenezewa leseni za gharama nafuu ili wafanyabiashara hao waweze kujikwamua kiuchumi na kukuza pato la Taifa.

Mabula amesema katika bunge la miswada linalotarajiwa kuanza Septemba mwaka huu jijini Dodoma, moja ya ajenda yake kuu ni kufikisha kilio cha wafanyabiashara wa wadogo wa filamu wanaotembeza filamu mtaani.

Kauli hiyo ameitoa wakati akizungumza na wafanyabiashara zaidi ya 300 wanaouza CD za kudurufiwa mtaani jijini hapa ambao wameitisha mkutano kwa ajili ya kuzungumza na wadau wa filamu kuhusu changamoto zinazowakabili.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.