ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, July 31, 2018

WAKAZI WA KANDA YA ZIWA SASA KUJISHINDIA MAMILIONI NA PEPSI.




GSENGOtV

Kampuni ya SBC Tanzania Limited, watengenezaji na wasambazaji wa vinywaji baridi aina ya Pepsi, Mirinda, 7up, Mountain Dew na Evervess, Mkoani  Mwanza wanayo furaha kuwaletea  Shindano kabambe litakalojulikana kwa jina la“Jishindie Mamilioni ”  Shindano hili  litahusu  soda aina ya Pepsi, Mirinda Orange, Mirinda Fruity, Mirinda Lemon, 7Up za ujazo wa mililita 350, na Mountain Dew (300ml).

Shindano hili litatangazwa Katika Radio, Magazeti, Mabango na Vipeperushi mbalimbali. Madhumuni ya kuwaletea shindano hili niKuboresha hali ya maisha ya wateja wetu wa kanda ya Ziwa kwa kuwapatia zawadi za fedha taslimu ili kuwawezesha kujikomboa kiuchumi.

Shindano hili litaendeshwa Kwa muda wa wiki sita kuanzia tarehe 01/08/18 hadi 16/09/18 katika mikoa ifuatayo: Mwanza, Shinyanga, Mara, Simiyu, Tabora, Geita, Kigoma na Kagera. 
 Meneja Mafunzo na Uwezeshaji SBC Tanzania Limited Rashid Chenja akionesha moja ya mabango ya kutambulisha shindano la Jishindie Mamilioni.
 Kutoka kushoto ni Phocas lusato Meneja Rasilimali watu SBC, akifuatia Meneja Mafunzo na Uwezeshaji SBC Tanzania Limited Rashid Chenja na Hussein Mkwawa ambaye ni Meneja mauzo Kanda ya Ziwa wakisikiliza vyema maswali ya waandishi wa habari (hawako pichani) katika utambulisho rasmi wa shindano la Jishindie Mamilioni, uliofanyika ukumbi wa mikutano SBC Nyakato jijini Mwanza.
 "Safiiiiii.....!!"

 Balozi wa PEPSI Albert Sengo (kulia) akitoa maelezo kwa wawezeshaji SBC, anayemsikiliza mbele yake ni Meneja Mauzo kanda ya Ziwa Hussein Mkwawa, Meneja Mafunzo na Uwezeshaji SBC Tanzania Limited Rashid Chenja na Meneja Rasilimali Watu Phocas Lusato  katika utambulisho wa shindano la Jishindie Mamilioni, uliofanyika ukumbi wa mikutano SBC Nyakato jijini Mwanza.
 "Hizi ndizo zawadi"
Nikama wakisemezana "Hebu tuone umepata nini ndani ya kizibo chako...." Balozi wa PEPSI Albert (kushoto) Sara Onesmo kutoka Clouds Tv na Johari Shani wa Mwananchi Communication.
 Shindano hili la“Jishindie Mamilioni” litakuana vizibo vya rangi ya Silva. Shindano hili litakua na zawadi nyingi za pesa taslimu kuanzia shilingi za Kitanzania 1,000,000/-, 500,000/-, 10,000/-, 5000/-,  1000/= na SODA YA BURE.

Ili Mteja ajishindie zawadi anatakiwa kununua soda za Jamii ya Pepsi kisha abandue ganda Ndani ya Kizibo akikuta maandishi aidha ya shilingi 1,000,000/-, 500,000/-, 10,000/-, 5,000/- 1000/-  au Free Pepsi (SODA YA BURE), atakua amejishindia zawadi hiyo papo hapo. 

Zawadi za shilingi 10,000/=, 5000/=,1000/=na Soda ya bure zitapatikana hapo hapo kwa aliyekuuzia soda, Gari ya Mauzo au Muuzaji wa Jumla. Vizibo vya zawadi vimeandikwa kwa rangi ya dhahabu, Zawadi za shilingi 1,000,000/-, 500,000/-  zitatolewa kiwandani Mwanza tu, Barabara ya Musoma, Nyakato, Kuanzia saa 4 asubuhi hadi saa 9 jioni siku za Jumatatu hadi Ijumaa (isipokua siku za sikukuu). 
Hii ndio fursa nzuri kwa wanywaji wa soda zetu kujishindia Mamilioni kila siku kwa kunywa Soda zetu, Kuna zawadi nyingi sana, kunywa sasa unaweza kuwa wewe ndio mshindi, ili uboreshe maisha yako.

Tarehe ya mwisho ya kutoa zawadi ni Tarehe 30 Septemba 2018.

Tuna imani utashirikiana nasi  kufanikisha shindano hili na kuboresha maisha yako.

“Jishindie Mamilioni ”


ASANTE SANA  

SBC  TANZANIA  LIMITED

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.