ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, July 13, 2018

RC MAKONDA AKABIDHI MWENGE WA UHURU KWA MKOA WA PWANI.


Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda leo July 12 amemkabidhi Mwenge wa Uhuru Mkuu wa mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo baada ya Mwenge huo kukamilisha shughuli ya uzinduzi na uwekaji wa mawe ya msingi kwenye miradi mbalimbali ya maendeleo yenye thamani ya zaidi ya shilingi Bilioni 32.

RC Makonda amesema kuwa ndani ya siku tano ambazo mwenge ulikuwa jijini Dar es salaam umefanikiwa kutembelea, kuweka mawe ya msingi na kuzindua miradi 36 ya maendeleo kwenye wilaya zote tano. 

Aidha RC Makonda amewashukuru wananchi wa Dar es salaam kwa ushirikiano mkubwa walioonyesha tangu siku mwenge ulipoingia hadi leo alipoukabidhi kwa mkoa wa Pwani.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.