ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, July 20, 2018

GUNDUA MENGI MTAANI KUPITIA KAMPENI YA FURAHA YANGU


Kampeni ya uhamasishaji watu kupima Afya imeendelea tena leo katika mitaa mbalimbali ya jiji la Mwanza, wilaya za Ilemela na Nyamagana zimehusishwa na mpango huo.
Mmoja wa balozi wa uhamasishaji kutoka mradi wa Furaha Yangu Bi. Zainab akitoa elimu ya kunini tunapaswa kupima na kuzijua afya zetu, na hapa ni katika eneo la kituo cha mabasi Nyakato Buzuruga jijini Mwanza.
Maswali ya kitaalamu yataulizwa jumamosi hii ya tarehe 21 viwanja vua Furahisha jijini Mwanza ambapo ndiko kwenye shughuli za upimaji na tiba kwa maradhi mbalimbali kama vile kifua kikuu, moyo, presha, upimaji wa vvu na magonjwa mengine.
Chakufurahisha suala hili limekuwa na mvuto kwa watu wa kila rika, nayo maswali hayakukosekana.
Uhamasishaji na uelimishaji kwa maswali madogo umefanyika sanjari na kuwahamasisha wadau kuibuka Jumamosi hii viwanja vya Furahisha jijini Mwanza.
Swali la kwanza, swali la pili na swali la............
Naam vijana nao wameukubali mpango huu wa kujua afya.
Katikati ya wadau.
Ubishi na ubishani hapa palinoga.
Bodaboda akajishindia kofia kwa kujibu vyema maswali.
Mama huyu alijishindia fuko la mama kwa kuhamasisha watu kujitokeza kupima akitumia lugha ya Kikerewe.
Wanafunzi nao wamevutiawa na mpango huu wa kupima.
Kamanda akajinyakulia zawadi ya Tshirt.
Vaaaa mwanangu.
Tokelezea.
Kofia kwa rasta.......
Pima Jitambue Ishi..........!!

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.