ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, June 7, 2018

BREAKING NEWS: WANANCHI 35 WATIWA MBARONI KWA KUCHOMA MOTO GARI LA ABIRA.


GSENGOtV


Jeshi la Polisi mkoa wa Mwanza limewatia mbaroni Wananchi thelathini na watano, kwa tuhuma ya kuliteketeza kwa moto gari la abiria aina ya Isuzu Journey, baada ya gari hilo kumgonga mtoto na kusababisha kifo chake katika eneo la kata ya Bugogwa wilayani Ilemela.

Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza Naibu Kamishna wa polisi Ahmed Msangi amemtaja mwanafunzi aliyefariki papo hapo kuwa ni Naomi Opio mwenye umri wa miaka 12 mwanafuzi wa darasa la nne katika shule ya msingi Kisundi, huku mdogo wake aitwaye Baton Opio mwenye umri wa miaka 9 anayesoma darasa la tatu katika shule hiyo akijeruhiwa kichwani na kuvunjika mkono wa kulia na amelazwa katika hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Mwanza Sekou toure kwa matibabu zaidi.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.