ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, June 18, 2018

BAKWATA MWANZA WADAI HAWATOKUBALI KUONEWA.


GSEBGOtV
BARAZA Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) limesema halitakubali kuonewa na watu wachache na limedhamiria kurejesha mali za Waislamu zilizohodhiwa kwa maslahi ya wachache.

Pia limesema waumini wa dini Kiislamu wameridhia kuwa chini ya kiongozi mmoja Sheikh Mkuu wa Tanzania na kuwataka wengine wote kufuata Katiba ya BAKWATA ili kuepusha vurugu.

Kauli hiyo ilitolewa ja juzi jijini Mwanza kwenye Baraza la Idd El Fitri na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya BAKWATA Taifa Sheikh Hassan Kabeke ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Kuendeleza Quraan na Suna Tanzania (JUQUSUTA).

Alisema BAKWATA hitakubali kuporwa mali za Waislamu na kuwanufaisha wachache ambao wamelifanya baraza hilo kuwa ombaomba wakati lina mtandao mkubwa kuliko taasisi nyingi za dini nchini kwa kuwa lina mtandao wa uongozi hadi vijijini.

Sheikh Kabeke alisema kuwa wamejipanga kurejesha mali za waislamu na kuwataka waumini na viongozi wa dini hiyo kuwa imara na wahakikishe mali zote za Waislamu zinarudishwa lakini wakilegea zote zitakwisha.“Tunataka BAKWATA yenye nguvu itakayopambana na watu wanaopuuza maelekezo ya baraza hilo na hatuna sababu ya kuwa ombaomba wakati tumeweka mizizi hadi vijijini, isipokuwa tunazidiwa na CCM tu.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.