ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, June 9, 2018

JEZI YA NIGERIA YAPEWA NAMBA MOJA KWA MVUTO LINAPOKUJA SUALA LA MITUPIO.


Mashabiki mbalimbali wa soka duniani, wamezichagua jezi za Nigeria kuwa namba moja kwa timu zinazoshiriki Kombe la Dunia.

Mashabiki hao kupitia mitandao mbalimbali ukiwemo ule wa Gazeti la Marca la Hispania, wametoa namba moja kwa jezi ya Nigeria kwamba inavutia sana.

Jezi inayofuatia kwa kuvutia ni lie ya Ufaransa ambayo mashabiki wameipa namba mvili na namba tatu imekwenda kwa Croatia.

Ujerumani imeshika nafasi ya nne, tano imekwenda kwa Iceland na ’namba sita ni Mexico.

Hivi karibuni, jezi za Nigeria zilizotengenezwa na Nike, zilinunuliwa kama njugu na kuzua gumzo kubwa.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.