ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, May 24, 2018

TUZO YA MCHEZAJI BORA LIGI KUU KUTOLEWA JUNI 23.


Tuzo ya Mchezaji Bora wa Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) Tanzania Bara inatarajiwakufanyika Juni 23 mwaka huu ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam.

Kufanyika kwa tuzo hizo ni utaratibu ambao Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limejiwekea kila mwaka baada ya kumalizika ligi kutoa tuzo kwa waliofanya vizuri kwa kushirikiana na Wadhamini wakuu wa VPL Kampuni ya Simu za mkononi ya Vodacom Plc na msimu huu tutakuwa na washirika wengine Azam Tv, Benki ya KCB na Premier Bet

Licha ya Tuzo ya Mchezaji Bora wa mwaka wa ligi, pia kunatolewa tuzo mbalimbali, ambapo kwa mwaka huu tuzo moja imeondolewa na nyingine imeongezwa ikiwa ni katika kuboresha.

Tuzo iliyoondolewa ni ya Mchezaji Bora wa Kigeni na imefanyika hivyo ili kuwapa fursa wachezaji wote kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL badala yakuwatenganisha.

Pia msimu huu imongezwa Tuzo ya Mwamuzi Bora Msaidizi ambayo haikuwepo msimu uliopita, hiyo ni kutokana kuthamini nafasi ya waamuzi wasaidizi.

Kwa mazingira hayo tuzo zitakazotolewa Juni 23, ambapo wadhamini wakuu ni Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom ni hizi zifuatazo:

Bingwa
Mshindi wa Pili
Mshindi wa Tatu
Mshindi wa Nne
 Mfungaji Bora
Timu yenye nidhamu
U20 Player (Tuzo ya Ismail Khalfan)
Mchezaji Bora Chipukizi
Mwamuzi Bora Msaidizi
Mwamuzi Bora
Kipa Bora
Kocha Bora
Goli Bora
VPL Best Eleven
Mchezaji wa heshima

Zawadi kwa kila kategori pamoja na majina ya wanaowania tuzo ukiacha bingwa, mshindi wa pili, wa tatu, wa nne na mfungaji bora ambao hujulikana kulingana na ligi inavyoendelea zitatangazwa siku za usoni.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.