ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, May 31, 2018

POLISI YA RWANDA YAWATAKA RAIA KUACHA KUINGIA HIFADHI ZA TANZANIA KINYEMELA ILI KUEPUKA MATATIZO.


CHANZO/PARStoday
Katika juhudi za kudumisha ujirani mwema kati ya Rwanda na Tanzania, serikali ya Kigali imewaonya raia wa taifa hilo hususan wale wanaoisho maeneo ya mashariki mwa nchi hiyo karibu na mpaka wa Tanzania kujiepusha na vitendo vya kuvuka mpaka kuingia nchi hiyo jirani.
Hii ni kwa kuwa raia hao wamekuwa wakivuka mpaka wa Rwanda na kuingia Tanzania kwa ajili ya kuwinda na kushenya kuni, kitendo ambacho kimekuwa na matokeo mabaya.

Askari wa kulinda hifadhi Tanzania wakiwapiga vikali watu wanaowakamata katika operesheni zao

Kwa mujibu wa maafisa wa polisi wa Rwanda, aghlabu ya Wanyarwanda wanaokamatwa na maafisa wa wanyamapori wa Watanzania huwa wanapigwa vibaya huku wengine wakipoteza maisha kabisa.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.