ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, May 21, 2018

JAFO AGUSWA NA JUHUDI ZA MAENDELEO NYAMAGANA


NA ZEPHANIA MANDIA/GSENGOtV.
Waziri wa tamisemi SULEIMAN JAFFO amempongeza mkurugenzi mtendaji, KIOMONI KIBAMBA, wa halmashauri ya jiji la Mwanza kwa kuridhishwa na miradi ya Halmashauri ya jiji la Mwanza.

Jaffo ametembelea miradi hiyo ikiwemo ukarabati wa shule kongwe ya wasichana Nganza sekondari.

Ziara ya waziri Jaffo jijini Mwanza inaanza kwa kukagua miradi mbalimbali iliyotekeleza katika halmasahuri hiyo, kubwa kati ya miradi hiyo ni utayari wa jiji hili kuona kuana haja ya kupunguza msongamano katika jiji hili kwa kutenga eneo la maegesho ya magari ya mizigo.

Hekari 23 zimetengwa katika eneo la buhongwa nje kidogo ya jiji la Mwanza lengo ikiwa ni kupunguza msongamano pamoja na kuengeza mapato kwa jiji hilo.

Akiwa katika eneo hilo JAFFO ameeleza kufurahishwa na hatua ya jiji la Mwanza kubuni mradi huo ambao utaongeza mapato kwa halmashauri na kupunguza msongamano katikati ya jiji.

Awali alianza kwa kukagua maboaresho ya shule ya wasichana ngaza ambapo zaidi ya shilingi milioni 900 zimatumika kuboresha shule hiyo ambayo kwasasa inakabiliwa na changamoto ya gari la kuhudumia wanafunzi.

Halmashauri ya jiji la mwanza limefanikiwa kuanzisha na kuboresha miradi mbalimbali ikiwemo ya afya,miundo mbinu ,elimu pamoja na machinjio ya kisasa ,huku ikiwa na malengo ya kuboresha stendi kuu ya mabasi nyegezi.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.