ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, May 12, 2018

HARMONIZE: AZUNGUMZIA BIFU LAKE NA MWARABU FIGHTER.


Msanii kutoka lebo ya WCB ambae wiki chache hapo nyuma kulikuwa na skendo za kuwa na usaliti kati yake na mpenzi wake sarah, ambapo ilisemakana kuwa mpenzi wake huyo anauhusiano na Baunsa wa Diamond Platnumz, anaeitwa Mwarabu Fighter.


Akizungumza na Host wa kipindi cha 'Kikwetu' kinachoruka kila Jumamosi ndani ya Jembe Fm Mwanza anayekwenda kwa jina la Natty E swali lilikuwa hivi:-

NATTY E BRANDY - Yajayo yanashtua sana, Eh bana ee watu wameniuliza maswali mengi sana ila swali kubwa wakasema nidili na ujumbe uliouandika mwenyewe Instagram ujumbe unasema "Mara kumi ningesikia Mboso anakula mzigo ningemsubiri paleeee........Yaani ile anaingia tu nikamuulia hapo hapo. Sasa mtu kama huyu mimi naanzaje kumuuliza maana hata kucheka tu kwa msimu jamani Mungu huyu"

Kwa hiyo wewe na Mwarabu Fighter hamuongei kwa sasa?

HARMONIZE :- Mwarabu, Mwarabu brother wangu kabisa.

NATTY E BRANDY :- Kwahiyo ile ni kiki au vitu gani?

HARMONIZE :- No unajua kuna watu ambao wanapenda kuongea vitu ambavyo hawavifahamu.....
 BOFYA PLAY HAPA CHINI KUSIKILIZA
Akiwa na warembo wa Miss Mwanza Harmonize hapa anajiachia jisongi 'Kwangwaru'
Warembo wa Miss Mwanza ndani ya studio za 93.7 Jembe Fm kwaajili ya mahojiano. 
Mwalimu wa warembo wa Kinyang'anyiro cha Miss Mwanza ambaye pia ni mtangazaji pia Dj wa 93.7 Jembe Fm Mustapha Kinkulah amesema ingawa bado mchakato wa usajili wa warembo unaendelea lakini mpaka sasa kuna muitikio mkubwa wa warembo kujitokeza na kuomba nafasi ya kushiriki.

"Siku za usoni baada ya kuingia kambini tunategemea kufanya mchujo kisha tutapata tui la maana, kwani tumedhamiria na tumepania kwamba Miss Tanzania safari hii lazima atokee Mwanza" Alisema Kinkulah.
Ushindani wa weredi ulihusishwa kupitia maswali yenye akili ........
Mrembo alipo ambiwa kununa........
 Leo Mei 12, Harmonize anatarajiwa kufanya makamuzi ya hatari kwenye viwanja hivyo vya Rock City Mall ndani ya show la kibabe la 'Hit Zone Turn Up' lililoandaliwa na kituo cha Redio Jembe Fm Mwanza, chini ya watangazaji wake Natty E Brandy, Babajuti na Deejay Jacko. Show hilo likipewa nguvu na Jembe ni Jembe.
 'Kwangwaru'

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.