ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, May 11, 2018

HARMONIZE APATA MAPOKEZI MAKUBWA MWANZA.

Msanii wa Bongo flava kutoka WCB Harmonize hatimaye amewasili jijini Mwanza kwa ajili ya kukata kiu ya mashabiki wake katika show iliyopangwa ikapangika ya HIT ZONE TURN UP.

Hit Zone ni kipindi cha burudani ya mipini ya vijana wa kisasa ambacho huruka hewani kila siku za juma saa 7 kamili mchana hadi 10 jioni kinataraji kuwakusanya mashabiki wake kula burudani pamoja ambapo pia moja kati ya shughuli zitakazo nogesha usik huo ni uzinduzi wa Mashindano ya Miss Mwanza na Lake zone.

Harmonize na mkewe wamefurahishwa na mapokezi hayo na kuwaomba mashabiki  wasikose kwani wamewandalia vitu vipya.

Harmonize anayetamba na kibao cha Kwangaru aliyemshirikisha Rais wa WCB Diamond, ameambatana na mkewe Sarah, na kupokelewa na baadhi ya washiriki wa mashindano ya Miss Mwanza.

Mashindano hayo yaliyoandaliwa na Mepal Management Wakala wa Miss Mwanza 2018 , yanatarajia kuzinduliwa hiyo kesho Mei 12 kwenye viwanja hivyo vya Rock City Mall.

Kiingilio ni shilingi 10,000/= tu 











Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.