ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, May 30, 2018

FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY WATOA SOMO KUELEKEA UCHAGUZI NCHINI

a
Mkurugenzi Mtendaji wa Foundation for Civil Society Bw. Francis Kiwanga akitoa ufafanuzi mbele ya wageni waalikwa mapema leo jijini Dar es salaam wakati akifungua  mkutano wa kujadili nafasi ya Asasi za kiraia katika chaguzi zijazo hapa nchini.

Asasi za kiraia nchini zimetakiwa kujitoa katika kuhakikisha wananchi wanashiriki kwa wingi katika chaguzi mbalimbali ikiwemo ya serikali za mitaa na wa serikali kuu wa mwaka 2020.

Hayo yamesemwa mapema leo Jijini Dar es salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Foundation for Civil Society Bw. Francis Kiwanga alipokuwa akifungua mkutano wa wadau wa uchaguzi, wenye lengo la kujadili hali ilivyo kabla ya kufikia uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika hapo mwakani.

Mzee Gallus Abeid kutoka Mwalimu Nyerere Foundation akichangia mjadala mapema leo jijini Dar es salaam katika Mkutano wa Uchaguzi ulioandaliwa na Shirika lisilo la kiserikali la Foundation for Civil Society.

Katika Mkutano uliowakutanisha wadau kutoka Asasi mbalimbali za Kiraia, Taasisi za elimu ya juu, vyama vya wafanyakazi, vyama vya dini mashirika yanayoshughulikia amani nchini  kujadili nafasi na wajibu wao kama azaki kuelekea chaguzi zijazo hapa nchini.
Bwana Kiwanga amesema kuwa ushiriki wa wananchi katika kupiga kura umekuwa ni mdogo sana kwani 2010 wamepiga asilimia 43 peke yake na kwa mwaka 2015 ni asilimia 67 ya wananchi wote wenye sifa za kupiga kura.

Baadhi ya washiriki kutoka asasi mbalimbali za kiraia wakifuatilia kwa umakini mkutano.

Ameeleza kuwa  hii inatokana na wananchi kutokuwa na imani na viongozi wanaochaguliwa kwani wanaamini hata usipopiga kura basi mgombea wa chama fulani atapita kwa njia yeyote ile, hivyo taasisi zinazohusika ikiwemo wizara ya tamisemi na NEC pamoja na ZEC kuboresha utendaji wao wa kazi ili kurejesha imani hiyo kwa wananchi.


Amesema  kuwa asasi za kiraia zina jukumu kubwa la kushirika katika mchakato kabla, kipindi chenyewe cha uchaguzi na baada ya uchaguzi kwa kuwapa hamasa wananchi lakini pia kuomba nafasi za uangalizi katika kipindi hicho.

Wageni waalikwa wakifuatilia mkutano kwa umakini.

Amesistiza uhalali wa kuwapata viongozi ambao ni matwakwa ya wananchi kwani hii inaweza kuleta kitu kizuri kwa kuwa atakuwa kapewa Baraka zote na wananchi na pia watashirikiana nae kwa hali na mali kwa kuwa wanajua ndio chaguo lao sahihi.
Kwa upande wake Mzee Gallus Abeid kutoka Mwalimu Nyerere Foundation amesisitiza uwepo wa amani katika kipindi cha uchaguzi na baada ya uchaguzi kwani amani ndio msingi wa mambo yote.

Baadhi ya washiriki wa mkutano wa uchaguzi ulioandaliwa na shirika la Foundation for Civil Society wakiwa katika picha ya pamoja mapema leo jijini Dar es salaam.

Amesema  kila mtu ana haki ya kuchagua na kuchaguliwa hivyo inapotokea watu wanamchagua mgombea Fulani alafu matokeo yanabadilishwa na kupewa mtu mwingine hii sio sawa na inaweza kutowesha amani ya nchi

Lakini pia hali ya mtu anatumia muda mwingi kwenye foleni ya kujiandikisha na mwisho wa siku anaenda kupiga kura anaambiwa jina lako halipo kwenye daftari hali hii inasababisha watu wengi kuacha kujiandikisha kupiga kura na kupoteza haki yao ya msingi.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.