ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, May 14, 2018

BREAKING NEWS: ELIZABETH MICHAEL AMEACHIWA HURU KUTOKA GEREZANI.


Leo May 14, 2018 Taarifa iliyotufikia muda huu ni kumhusu Muigizaji wa filamu nchini, Elizabeth Michael maarufu Lulu, amebadilishiwa adhabu kwa amri ya Mahakama Kuu ya Tanzania na sasa atatumikia kifungo cha nje.

Lulu alihukumiwa kifungo cha miaka miwili gerezani baada ya kupatikana na hatia ya kuua bila kukusudia.

Hukumu ya kesi hiyo ilisomwa na Jaji wa Mahakama Kuu, Sam Rumanyika, ambaye baada ya kusikiliza utetezi kutoka kwa mawakili wa upande wa mshtakiwa alitoa hukumu.

Lulu, alishtakiwa kwa kesi ya kumuua bila kukusudia, aliyekuwa muigizaji maarufu wa filamu nchini na nje ya nchi, Steven Kanumba ambaye pia alikuwa mpenzi wake.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.