ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, April 25, 2018

KUTANA NA MAMA MPARA SAMAKI ANAJIITA 'SURA YA BABA SHAROBARO ALIYEPINDA'


Uvuvi ni moja ya shughuli kubwa inayofanyika katika Ziwa Victoria. Sekta hii ya uvuvi inachangia asilimia saba ya uchumi wa mkoa kwa mujibu wa tovuti ya mkoa. 

Inaelezwa kwamba shughuli za uvuvi ndizo zinazoongoza katika kuingiza fedha za kigeni katika mkoa huu na kwa mujibu wa utafiti wa mwaka 2011, mkoa ulikuwa na jumla ya wavuvi 52,942 huku boti na mitumbwi ikiwa 14,480.

Ili samaki aingie sokoni kwa walaji hana budi kutayarishwa, na hatua ya kwanza ya matayarisho ni kuondoshwa magamba twaita 'Kupara samaki'

Ukifika mwalo wa Kamanga uliopo wilayani Nyamagana mkoani Mwanza utakuta makundi kwa makundi wanawake na wanaume vijana wakiwa nyuma ya meza zao za kupara samaki, wakiwa 'bize' na harakati za kuhakikisha kuwa wanakamilisha huduma husika.

VIELELEZO:-
Ni kielelezo tosha kwamba hii ni ajira sasa.
Nini changamoto za wadau hawa?
Wanakutana na nini?
Jeh utamtambuaje samaki aliye china?
Jeh samaki aliyevuliwa kwa sumu anajulikana?

Kutana na mwanamama huyu maarufu kwa jina la 'Sura ya Baba' 'Sharobaro aliyepinda' msikilize ujifunze kitu katika KAZI DARASA


Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.