ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, April 27, 2018

HAFLA YA KUMUAGA ALIYEKUWA KATIBU TAWALA MKOA WA MWANZA.

Aliyekuwa Katibu Tawala Mkoa Mwanza, Kamishna wa Polisi Clodwig Mtweve mara baada ya kukabidhi ofisi amefanyiwa sherehe ya kuagwa na watumishi aliofanya nao kazi kwa ukaribu kwa kipindi chote cha ajira, shughuli iliyofanyika katika bustani za Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza.
Kamishna Mtweve amekabidhi majukumu ya ofisi kwa Kaimu Katibu Tawala mkoani Mwanza, Mhandisi Warioba Sanya mbele ya Mkuu wa Mkoa Mwanza, Mhe.John Mongella, Kamati ya Ulinzi na Usalama mkoani Mwanza pamoja na watumishi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mwanza.
Hafla ya kumuaga Kamishna Mtweve imefanyika jumatano ya Aprili 25, 2018.
Rais John Pombe Magufuli alimteua Kamishna wa Polisi, Clodwing Mtweve mwishoni mwa mwezi Januari mwaka 2016 kuwa Katibu Tawala mkoani Mwanza ili kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Faisal Issa ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.
Kabla ya Uteuzi huo Kamishna Mtweve alikuwa Kamishna wa fedha na Utawala wa Jeshi la Polisi Tanzania.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.