ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, April 11, 2018

JUHUDI ZA KUIFIKIA SERIKALI YA VIWANDA KWA JIJI LA MWANZA ZAPIGWA TAFU NA BENKI ABC

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mangella wakati alipokuwa akizindua tawi jipya la Benki ABC jijini Mwanza.
 NA ZEPHANIA MANDIA WA GSENGO TV
Ili kufikia adhma ya Serikali ya Viwanda wawekezaji wa ndani na nje wametakiwa kuendelea kuwekeza mkoani Mwaza kwa kubuni miradi endelevu kulingana na jiografia ya rasilimali zilizomo ili kukuza uchumi wa nchi.
Hayo yamesemwa mapema hii leo na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mangella wakati alipokuwa akizindua tawi jipya la Benki ABC jijini hapa.

 Dona Botha, ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ABC nchini anayemaliza muda wake amesema kuwa, pamoja na kuendelea kubuni bidhaa mbalimbali na zenye kuzingatia mahitaji halisi ya soko kwa wateja wake Benki ABC ni benki inayoongoza nchini Tanzania katika huduma ya uhamishaji mihamala ya fedha na ufanyaji manunuzi kwa njia ya mitandao kwa uhakika.


Imman John (pichani kulia), ni Mkurugezi wa Fedha ambaye anayekwenda kukabidhiwa nafasi ya Ukurugenzi Mtendaji, kwa upande wake, amewataka wananchi kuzichangamkia fursa za benki hiyo ikiwa ni pamoja na kuchukuwa mikopo yenye riba nafuu na kuweka akiba kwaajili ya miradi na shughuli mbalimbali za maendeleo.


Bi. Joyce Malai 
 Kwa upande wake Mkuu wa kitengo cha wateja wakubwa na wadogo Bi. Joyce Malai amesema kuwa licha ya benki hiyo kutoa huduma za kawaida, pia imeboresha huduma zake kwa kutoa huduma kwa  kila mtanzania hasa kwa wale wasio na akaunti za Benki, kwa kutoa huduma za kifedha kupitia wakala wa taasisi mbalimbali nchini inayowezesha wateja wake kupata huduma za benki hiyo wakiwa wakiwa popote nchini.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mangella akiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ABC Dona Botha pamoja na Mkurugenzi wa Fedha Imman John (kulia) kwa pamoja wakizindua jiwe la tawi linaloashiria ufunguzi huo jijini hapa.
Pongezi kwa kazi nzuri.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mangella akikagua huduma na mazingira ya tawi jipya la Benki ABC jijini hapa.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mangella akiwa ameshikilia card ya ATM ya baada ya kufungua akaunti katika tawi jipya la Benki ABC.
Hapa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mangella akipata maelezo kutoka kwa Bi. Joyce Malai  ambaye ni Mkuu wa kitengo cha wateja wakubwa na wadogo wakati alipokuwa akizindua tawi jipya la Benki ABC jijini hapa.
Mazingira ya benki na jiografia yake.
Safu ya Benki ABC.
Picha ya pamoja.
                                                                  Picha ya pamoja.


Benki ABC ambayo ni moja ya kampuni tanzu za Atlas Mara, inayopatikana sasa katika nchi saba barani Afrika, huku ikijivunia kuwa na tuzo ya kuwa Benki bora Afrika kwa mwaka 2017 ambapo bado imeendelea kujidhatiti na kuenea zaidi hapa nchini kwa kufungua matawi mengi zaidi ambapo mara baada ya kuzindua tawi hili la Mwanza sasa inajiandaa kuelekea mkoani Dodoma ambako nako inakwenda kuzindua tawi lake.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.