ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, April 27, 2018

BREAKING NEWS: MDOGO WA JOHN HENCE AUAWA KWA KUCHOMWA KISU.

Mdogo wa Mbunge wa John Heche anayejulikana kwa jina la Suguta, ameuawa kwa kuchomwa kisu.

Kwa mujibu wa John Heche mdogo wake amechomwa kisu na polisi wa kituo cha Sirari waliomkamata baada ya kumkuta bar akinywa pombe, huku akiwa na pingu mkononi.

"Ni kweli kwamba mdogo wangu ameuawa na polisi, na ameuawa akiwa mikononi mwa polisi, jana usiku polisi walimkamata akiwa kwenye bar alikuwa na wenzake wanakunywa pombe, sasa wakamkamata, wameenda naye mpaka kituo cha polisi akiwa mzima wamemfunga pingu, askari mmoja akatoa kisu akamchoma eneo la mgongo kikaenda mpaka kikagusa chembe ya moyo, wamemchoma kisu akiwa wamemfunga pingu tena akiwa kituo cha polisi", amesema John Heche.


Mwili wa kijana huyo umehifadhiwa katika (Mortuary) ya Tarime.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.