ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, April 23, 2018

NYUMBA ZAIDI YA 40 ZAHARIBIWA NA MVUA KUBWA KILIMANJARO

Nyumba 40 zimeharibiwa na mvua kubwa zilizonyesha katika Kijiji cha Kileo Wilaya ya Mwanga Mkoani Kilimanjaro , nyumba kumi zimeanguka na zingine 30 kukatika kwa nyufa huku baadhi ya nyumba zikiwa zimengirwa na maji katika kijiji hicho.

Baadhi ya wananchi walioathiriwa na tukio hilo wamesema, tetemeko, radi na mvua hiyo ilianza saa nane za usiku wa kuamkia jana lakini kwa bahati nzuri hakuna aliyejeruhiwa baada ya kuwahi kujiokoa.

kufuatia hali hiyo ‘waathirika hao wakiwemo wanawake  Bi Kaweresia Akilimali  na Bi. Mwajuma Amir  wameiomba serikali wilayani mwanga kuwapatia msaada wa haraka wa kurejesha nyumba zao katika hali ya kawaida kutokana na uwezo mdogo walionao wa kipato.

Mwenyekiti wa serikali ya kijiji hicho Bw Kazeni Mcharo amesema kaya za nyumba hizo  awali zilihifadhiwa kwenye shule za sekondari za msingi za kijiji hicho lakini sasa wamechukuliwa na ndugu na jamaa kwa muda...insert ya bw kazeni mcharo mwenyekiti wa kijiji cha kileo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.