ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, March 15, 2018

RAIS TRUMP AMTEUA MTANGAZAJI WA TELEVISHENI KUWA MSHAURI MKUU WA UCHUMI.


Trump amteua Kudlow kuwa mshauri mkuu wa masuala ya uchumi. Mchambuzi wa masuala ya fedha katika televisheni nchini Marekani, Larry Kudlow sasa atakuwa mshauri mkuu mpya wa masuala ya uchumi katika Ikulu ya Marekani ya White house.

Kudlow amelieleza shirika la habari la AP kuwa amekubaliana na uteuzi huo wa rais Donald Trump kuhudumu kama mshauri wa masuala ya uchumi. Kudlow atachukua nafasi ya Gary Cohn ambaye alitangaza wiki iliyopita kuwa atajiuzulu nafasi hiyo baada ya kupinga mipango ya rais Donald Trump inayohusiana na viwango vipya vya kodi kibiashara. Kudlow mwenye umri wa miaka 70 ni mchambuzi mwandamizi katika kituo cha Televisheni cha CNBC.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.