ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, February 22, 2018

VIDEO YA DC.KWIMBA AKABIDHI KWA WAIMBAJI WA AICT NGUDU WANAOKWENDA NCHINI RWANDA KUITANGAZA AMANI.



NA ZEPHANIA MANDIA WA G.SENGO TV.
Mkuu wa wilaya ya kwimba Mtemi safiri,amewakabidhi Bendera ya Taifa wanakwaya ya AICT Ngudu mjini wakijiandaa kwenda nchini Rwanda kuitangaza amani kupitia neno la Mungu kwa njia ya injili.

Ni wakati huo huo ambapo, Umoja wa makanisa ya kikristo(CCT)kata ya Ngudu wilayani Kwimba mkoani Mwanza ukitumia hafla hiyo kulaani hatua ya baadhi ya wananchi wachache wa kata hiyo, kuusimamisha msafara wa waziri mkuu KASIMU MAJALIWA kushinikiza kuondolewa kwa mkuu wa wilaya hiyo mhandisi MTEMI SEMEON.

Mwenyekiti wa umoja huo Mchungaji SAIMON CHEM amesema kuwa madai ya baadhi ya wananchi kuwa mkuu wa wilaya hiyo amekuwa akiwaamrisha polisi kuwakamata kwa kisingizio cha uzururaji na kisha kuwalimisha kwenye shamba lake si ya kweli.

Mwenyekiti wa chama cha wafanyabiashara,wakulima na wenye viwanda(TCCIA)wilayani kwimba RENATUS MAGENI akabainisha kiini cha sintofahamu iliyojitokeza.

Sakata hilo pia limemwibua mwenyekiti wa chama cha ACT-WAZALENDO wilayani kwimba GASTUS LUSIMBYA.

Viongozi hao wametoa tamko hilo wakati wa hafla ya kukabidhi bendera ya taifa kwa wanakwaya wa kanisa la AICT la mjini ngudu wanaokwenda kuliwakilisha taifa katika uimbaji nchini Rwanda. 

Akikabidhi bendera hiyo, mkuu wa wilaya Kwimba MTEMI SEMEON amewataka waimbaji hao kuwa mabalozi wazuri na kuwa kielelezo halisi cha Taifa linalosifika kwa amani duniani.





Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.