ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, February 23, 2018

MHE BITEKO: "MULUGO WEWE NI NOMA...!"

 
Naibu Waziri wa wizara ya madini Mhe Doto Mashaka Biteko (Kushoto) akizungumza jambo na Mbunge wa Jimbo la Songwe Mhe Philiph Mulugo wakati wa mkutano na wachimbaji wadogo uliofanyika katika kijiji na kata ya Saza, Wilaya na Mkoa wa Songwe, Leo 22 Februari 2018. Picha Zote Na Mathias Canal-Wazo Huru Blog
Baadhi ya wachimbaji wadogo wakimsikiliza Naibu Waziri wa wizara ya madini Mhe Doto Mashaka Biteko wakati wa mkutano na wachimbaji wadogo uliofanyika katika kijiji na kata ya Saza, Wilaya na Mkoa wa Songwe, Leo 22 Februari 2018.
Naibu Waziri wa wizara ya madini Mhe Doto Mashaka Biteko akisisitiza jambo wakati wa mkutano na wachimbaji wadogo uliofanyika katika kijiji na kata ya Saza, Wilaya na Mkoa wa Songwe, Leo 22 Februari 2018.

Na Mathias Canal, Songwe

Naibu Waziri wa wizara ya madini Mhe Doto Mashaka Biteko amesifu juhudi za mbunge wa Jimbo la Songwe Mhe Philiph Mulugo kutokana na uwajibikaji mkubwa katika kuwasemea wananchi wa jimbo hilo hususani katika kuimarisha uchumi wa wananchi kupitia sekta ya Madini.

Mhe Biteko ametoa pongezi hizo kwa mbunge huyo wakati akihutubia mamia ya wananchi waliohudhuria katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji na Kata ya Saza akiwa katika siku ya kwanza ya ziara yake Mkoani Songwe.

Naibu waziri huyo alisema kuwa mbunge huyo amekuwa mstari wa mbele katika kuwatetea wananchi wake hususani katika kuchochea shughuli za maendeleo ili kuongeza ufanisi wa maendeleo endelevu ya mtu mmoja mmoja na jamii kwa ujumla wake.

Pongezi hizo zinajili wakati ambapo mbunge Mulugo amefanikiwa kutatua mgogoro uliodumu kwa muda mrefu kati ya kikundi cha TUJIKOMBE na Kampuni ya Bafex kwenye eneo la uchimbaji dhahabu la mlima Elizabeth.

Katika kumaliza mgogoro huo kampuni ya Bafex imekubali kugharamia mradi utakaochaguliwa na kikundi hicho kama fidia ya gharama walizozitumia wachimbaji hao kuendeleza eneo hilo.

"Mheshimiwa Mulugo wewe ni hazina ya Songwe, namuomba Mungu aendelee kukutunza kwaajili ya watu hawa. Mimi nipo Bungeni muda wote wewe ajenda yako ni watu wako na unafanya hivyo bila kuchoka. Kwakweli wewe ni NOMA" Alisema Mhe. Biteko huku akishangiliwa na mamia ya wananchi waliohudhuria mkutano huo.

Sambamba na hayo pia amempongeza Mbunge huyo kwa ushirikiano mzuri baina yake na serikali ya Wilaya pamoja na Chama Cha Mapinduzi jambo ambapo linaakisi uwajibikaji wa serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli.

Alisema kuwa kilio hicho cha wananchi kimedumu kwa muda mrefu hivyo jukumu la serikali ni kutatua kero za wananchi sio kuchochea migogoro.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.