ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, February 17, 2018

KINONDONI, SIHA WAAAMUA.

ZOEZI la upigaji kura katika Uchaguzi Mdogo wa Ubunge na Udiwani katika baadhi ya maeneo, Tanzania Bara limeanza limeanza rasmi asubuhi hii ya leo tarehe Februari 17, 2018 ambapo majimbo mawili ya Kinondoni jijini Dar es Salaam na Siha mkoani Kilimanjaro yatakuwa kwenye mchakato wa kuwachagua wabunge wao baada ya waliokuwepo kujiuzulu.

Vile vile, uchaguzi huo utafanyika kwa Madiwani katika Kata nane Tanzania Bara na kuhusisha wapiga kura 355,131 walioandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na kutakuwa na vituo vya kupigia kura 867.

Vituo vya kupigia kura vimefunguliwa mapema leo asubuhi saa 2:00 huku wananchi wakijitokeza kuchagua viongozi wawakilishi wao na ulinzi ukiwa umeimarishwa na jeshi la polisi.

Katika Jimbo la Kinondoni, Said Mtulia wa CCM anachuana na Salum Mwalimu wa Chadema ambapo Siha, Elvis Christopher Mosi wa Chadema akichuana na Dkt. Godwin Ole Mollel wa CCM.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.